• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

KAMATI ya Siasa Mkoa wa Ruvuma yaridhishwa na ujenzi wa jengo la upasuaji kituo cha Afya Kindimbachini

Imewekwa kuanzia tarehe: July 1st, 2020

KAMATI ya Siasa ya CCM Mkoa wa Ruvuma ikiongozwa na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Musa Homera imeendelea na ziara ya kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo  katika Mkoa wa Ruvuma.

Kamati hiyo imekagua ujenzi wa jengo la upasuaji na ukarabati wa jengo la wagonjwa wa nje (OPD) katika kituo cha afya Kindimbachini kata ya Muungano Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga na kuridhishwa na hatua ya utekelezaji wa mradi huo ambao utawaondolea kero wananchi kusafiri umbali wa zaidi ya kilometa 120 kutafuta huduma ya upasuaji .

Akisoma taarifa ya mradi huo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Juma Mnwele  amesema mradi wa jengo la upasuaji ulianza mwaka 2016 na kwamba wananchi walihamasika kuchangia ujenzi huo na ambapo gharama za mradi hadi utakapokamilika  na vifaa ni zaidi ya milioni 72.

Akizungumzia ukarabati wa jengo la wagonjwa wa nje,Mkurugenzi huyo amesema,ukarabati unaendelea vizuri na kwamba gharama za ukarabati wa jengo hilo ni milioni 34, fedha hizo zinatokana na ruzuku ya afya ya mfuko wa pamoja kwa ajili ya matokeo ya ufanisi.

“Mradi wa jengo la upasuaji upo katika hatua za umaliziaji,pia ukarabati wa jengo la wagonjwa wa nje unaendelea vizuri,mradi huu utanufaisha wananchi wote wa kata za Muungano na maeneo jirani ya kata ya Namswea,Ruanda na Litumbandyosi’’,alisema.

Uchunguzi umebaini kuwa katika kata hizo hakuna kituo cha afya cha serikali hivyo wananchi kwa miaka mingi  wanakosa huduma muhimu kama ya upasuaji ambayo sasa wataipata katika kituo cha afya Kindimbachini.

Hata hivyo Mnwele anaitaja changamoto kubwa inayowakabili wananchi wa kata hiyo kuwa ni ubovu wa barabara ambayo kipindi cha masika inaweza kusababisha madhara kwa uhai wa mgonjwa anayehitaji huduma za rufaa katika hospitali kubwa na ukosefu wa huduma nyingine za kijamii kama umeme na maji.

Akizungumza mara baada  ya kukagua mradi huo Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Musa Homera amewapongeza wananchi wa Kindimbachini kwa kusimamia vema mradi huo ambao amesema unakwenda kuondoa kero ya huduma ya upasuaji ambayo wananchi wameipata kwa miaka mingi.

Naye Katibu wa CCM Mkoa wa Ruvuma Nuru Ngeleja amewataka wananchi wa Kindimbachini ili kumtia moyo Rais Dkt.John Magufuli  wajitokeze kwa wingi kumchangua  Rais,wabunge na madiwani katika uchaguzi mkuu mwaka huu kwa kuwapa kura zote za ndiyo.

Imeadikwa na Albano Midelo

Afisa Habari wa Mkoa wa Ruvuma

Julai mosi,2020

Mbinga

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • BODI ya kwanza ya maji yazinduliwa Tunduru

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.