• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

KAMATI ya Siasa ya CCM Ruvuma yaagiza watendaji Namtumbo kufanya marekebisho hifadhi za Jumuiya za Mbarang'andu na Kimbanda

Imewekwa kuanzia tarehe: July 4th, 2020

KAMATI ya Siasa ya CCM Mkoa wa Ruvuma imewaagiza watendaji wa serikali wilayani Namtumbo kufanya marekebisho ya mapitio katika hifadhi Jamii za Jumuiya  za Mbarang’andu na Kindamba kabla ya Agosti 30 mwaka huu.

Maagizo hayo yametolewa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Oddo Mwisho wakati anazungumza na wananchi wa kijiji cha Mchomoro wilayani Namtumbo,baada ya kukagua hifadhi ya Jumuiya ya Mbarang’andu ambayo wananchi wamekuwa wanalalamika kutotendewa haki na baadhi ya  watendaji wa hifadhi hiyo.

Mwisho  amesema utaratibu wa serikali katika hifadhi za jumuiya za kijamii inatakiwa kufanyiwa mapitio na marekebisho kila baada ya miaka kumi ambapo katika hifadhi hizo jambo hilo halijafanyika kwa miaka saba katika hifadhi ya Mbarang’andu na miaka miwili katika hifadhi ya Kindamba hivyo kulenga mgogoro baina ya serikali na wananchi.

Amesema hifadhi za jamii hizo zinazozungukwa na vijiji 15 ni muhimu kwa uhifadhi endelevu kwa  watanzania wote kwa kuwa zinahifadhi mazingira na kuepusha nchi yetu kugeuka jangwa na kusababisha ukame.

Hata hivyo Mwisho ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Ruvuma amesema baada ya kupata taarifa kuwa watendaji wa Wizara husika hawajafanya mapitio kulingana na makubaliano na sheria ndipo waliamua kufanya ziara ya ukaguzi wa maeneo hayo na kuamua kutoa maagizo kama chama tawala ambacho kinaongoza serikali.

“Wananchi walioingia kulima kwenye hifadhi wana makosa na watendaji wa serikali walioshindwa kufanya marekebisho ya hifadhi kwa mujibu wa sheria wana makosa kwa sababu hifadhi zilipaswa kufanyiwa mapitio upya kila baada ya miaka kumi  kulingana na makubaliano ya serikali na wananchi wenye maeneo ya hifadhi’’,alisisitiza.

Amesisitiza kuwa ifikapo Agosti 30 mwaka huu wamekubaliana na watendaji wa serikali marekebisho ya hifadhi yawe yamefanyika na kwamba wamekubaliana pia viongozi wa Jumuiya hizo ambao wapo madarakani kwa miaka 17 kinyume cha sheria waondolewe na uchaguzi ufanyike wa kuwapata viongozi wengine wapya.  

Mwisho amesisitiza kuwa watendaji wa serikali wapite katika vijiji vyote 15 vinavyozunguka hifadhi hizo na kufikia makubaliano  mapya ya mapitio ya hifadhi hizo na kuingia makubaliano mapya kuzunguka hifadhi hizo.

Ameagiza wananchi waliovamia hifadhi kwa kulima mpunga ndani ya hifadhi wajitokeze ili watambuliwe na ikiwezekana mazao ambayo wamenyang’anywa na watendaji wa hifadhi yarudishwe kwa wananchi.

Mwenyekiti huyu wa CCM Mkoa wa Ruvuma amesema lengo ni kukomesha uvamizi kwenye maeneo ya hifadhi hizo,hivyo wananchi wasiogope kujitokeza kuhofia kukamatwa kwa sababu Kamati imekubaliana na wahifadhi kuwa  waliochukuliwa mazao watambuliwe na kwamba wasirudie tena kulima kwenye hifadhi baada ya kumaliza mgogoro huo.

Mwisho amesisitiza kuwa kinachofanywa na Kamati ya Siasa ya Mkoa ni kutekeleza maagizo ya Rais Dkt John Magufuli   ya kwenda kwa wananchi na kuona maeneo yenye mgogoro yakoje jambo ambalo halijafanyika kwenye hifadhi za Mbarang’andu na Kimbanda.

Amesema serikali ikishatekeleza maelekezo ya Julai 12 mwaka huu kuhusu kuwarudishia mazao ya mpunga wananchi ambao walichukuliwa mazao yao baada ya kulima kwenye maeneo ya hifadhi,kamati ya Siasa  itarudi tena kwenye eneo la hifadhi na kuwaambia wananchi wasirudie kulima tena hadi hapo mapitio ya hifadhi yatakapofanyika.

Afisa Maliasili wa Halmashauri ya Wilaya Namtumbo Erenest Nombo amesema ni kweli kuna wananchi walivamia na kulima eneo la hifadhi za Mbarang’andu na Kimbanda kinyume cha sheria za uhifadhi ambao baadhi wamekamatwa na kesi zipo mahakamani na  mazao yao yamechukuliwa na serikali ambapo hadi sasa kuna magunia zaidi ya 100 ya mpunga.

Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo Adeni Nchimbi ameahidi kutekeleza yote yaliyoagizwa na Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa ili kumaliza migogoro baina na serikali na wananchi wanaozunguka hifadhi hizo.

Mmoja wa wananchi wa kijiji cha Mchomoro Said Huseni akizungumza baada ya maelekezo ya Kamati kwa niaba ya wananchi wenzake,amekishukuru Chama na  serikali kuridhia kufanyika mapitio  katika hifadhi hizo hali ambayo itaondoa migogoro baina ya serikali na wananchi ambayo imedumu kwa miaka mingi.

Amesema idadi ya wananchi katika vijiji vinavyozunguka hifadhi imeongezeka,ametolea mfano katika kijiji cha Mchomoro wakati yanafanyika makubaliano ya kwanza,kijiji kilikuwa na watu 6,000 ambapo hivi sasa idadi ya watu inakaribia 30,000 hivyo kuna changamoto ya ardhi.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma                                          

Julai 4,2020

Namtumbo      

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.