• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

KAMATI ya Siasa ya CCM Ruvuma yatoa wiki moja mradi wa maji Madaba kutoa maji

Imewekwa kuanzia tarehe: April 20th, 2021

KAMATI ya Siasa ya CCM Mkoa wa Ruvuma imetoa wiki moja kwa TANESCO kuhakikisha wanapeleka umeme kwenye mradi wa maji Madaba wilayani Songea ili wananchi waanze kunufaika na maji safi na salama.

Akizungumza baada ya kamati hiyo kukagua mradi wa maji Madaba ambao serikali imetoa zaidi ya shilingi bilioni mbili kutekeleza mradi huo,Mwenyekiti wa Kamati hiyo Oddo Mwisho amesema mradi huo umechukua muda mrefu ambapo hivi sasa serikali imedhamiria wananchi wa Madaba kupata maji na salama.

“Nampongeza Meneja wa RUWASA Mkoa wa Ruvuma ambaye ndani ya muda mfupi amesimamia miradi mingi ya maji iliyosababisha Mkoa wa Ruvuma kupata tuzo ya umahiri wa kusimamia miradi ya maji’’,alisema Mwisho.

Kwa niaba ya Kamati, Mwisho amewaagiza TANESCO Ruvuma kuhakikisha wanashughulikia umeme ili kuanzia wiki ijayo wananchi wa Madaba waanze kupata maji na kwamba Kamati ya Siasa haihitaji ubabaishaji katika kushughulikia suala ya kero ya maji kwa wananchi.

Kwa upande wake Mjumbe wa Kamati hiyo ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme ameutaja mradi wa maji Madaba kuwa ni wa zamani na kwamba wananchi wamepata shida kwa muda mrefu.

Hata hivyo amesema RUWASA Mkoa wa Ruvuma wamefanya kazi kubwa  ya kutekeleza mradi huo ambao upo katika hatua za mwisho kukamilika kwa asilimia 100.

Hata hivyo Mndeme amesema TANESCO wamechangia kuchelewesha mradi huo ambapo ametoa siku tano kuhakikisha wanamaliza kazi ya kupeleka umeme kwenye mradi huo na pasiwepo na kisingizio chochote.

“Wananchi wa Madaba hivi sasa wanahitaji maji,mimi nitapita hapa Alhamis,nikifika TANESCO hamjafanyakazi nitawaweka ndani wote,nataka tumalize huu mradi,TANESCO mkinizingua,tutazinguana,kila mtu avae sura ya kazi’’,alisisitiza Mndeme.

Awali Meneja wa RUWASA Wilaya ya Songea Mathias Charles  amesema mradi huo hadi sasa umefikia zaidi ya asilimia 90 ambapo amezitaja kazi zilizokamilika kwa asilimia 100 ni ujenzi wa tanki la juu la kuhifadhia maji kwenye kijiji cha Lituta lenye ujazo wa lita 50,000.

Kazi nyingine zilizokamilika ni ujenzi wa tanki la kuhifadhia maji katika kijiji cha Kipingo lenye ujazo wa lita 100,000 na kwamba ujenzi wa vituo 21 kati ya 40 vya kuchotea maji vimekamilika na ununuzi wa vifaa mbalimbali vya ujenzi umekamilika  kwa asilimia 98.

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Olaph Pilly kwa niaba ya wananchi wa Madaba ameipongeza serikali kwa kutekeleza mradi huo wa maji ambao utaifanya kero ya maji Madaba kubakia historia.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Aprili 19,2021

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.