• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

KAMATI za miradi Songea zatakiwa kusimamia miradi kikamlifu

Imewekwa kuanzia tarehe: March 17th, 2023

MWENYEKITI wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma Mheshimiwa Menas Komba amezitaka kamati zinazosimamia miradi katika ngazi ya Kata na Kijiji kushiriki kikamilifu kusimamia miradi inayotekelezwa kwenye maeneo yao.

Ameyasema hayo katika kikao cha kutoa mafunzo kwa kamati za ujenzi kwa Kata ambazo zimepokea fedha za kutekeleza miradi kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri Lundusi-Peramiho.

Pia lengo la kikao ni kuzitambua kamati ambapo wataalamu kutoka Idara ya ujenzi na manunuzi wametoa mafunzo namna ambavyo kamati zinatakiwa kutekeleza majukumu yake.

Akizungumza Mheshimiwa Komba amewataka wanakamati kujiepusha na vitendo vya hujuma ambavyo vitakwamisha miradi kutokukamilika kwa wakati au utekelezaji wake kuwa chini ya viwango.

Ameongeza kuwa katika ujenzi wa miradi hiyo uzalendo ni kitu cha muhimu hivyo amezitaka kamati za ujenzi kwa kushirikiana na Viongozi wa Kata na Vijiji pale ambapo nguvu za wananchi zinahitajika basi waweze kuwashirikisha na kuwasisitiza ili washiriki kikamilifu.

``Kamati ambazo mnaenda kusimamia ujenzi mkawe makini sana katika kuwasimamia mafundi viongozi hakikisheni kila fundi anaandaa mpango kazi kwani itasaidia sana kujua utendaji kazi wao pia miradi itakwenda kukamilika kwa wakati’’, amesisitiza Mheshimiwa Komba.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi  wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Bi Bumi Kasege amewataka mafundi viongozi kushiriki ujenzi kuanzia mwanzo hadi mradi utakapokamilika na sio kuwaachia mafundi wasaidizi ambao wanaweza wasiwe wataalamu na mradi usikamilike kwa viwango vinavyotakiwa.

Vilevile amezisisitiza kamati kununua na kutumia vifaa vyenye viwango vinavyokubaliwa na Serikali na kama ambavyo vimeelekezwa kwenye muongozo wa BOQ.

Nae mtaalamu kutoka ofisi ya TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Bw Patrick Mtavangu amezitaka kamati kutokutengeneza nyaraka za uongo kwa lengo la kumdanganya mwajiri kwani ni kosa hivyo amewahasa kuwa waaminifu katika kusimamia miradi hiyo na wasiwe chanzo cha kukwamisha miradi.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.