• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

KANISA latoa msaada wa vifaa tiba kwa zahanati Tunduru

Imewekwa kuanzia tarehe: September 20th, 2023

ZAHANATI ya kijiji cha Njenga kata ya Mchoteka Halmashauri ya wilaya Tunduru mkoani Ruvuma,imepokea msaada wa vifaa mbalimbali kutoka kwa Kanisa la Upendo wa Kristo Masihi vitakavyosaidia  utoaji wa huduma bora kwa wananchi.

Vifaa vilivyotolewa na kanisa hilo ni vitanda  vya kulala  watu wazima,vitanda vya kujifungulia vitanda kwa watoto wadogo na viti vya magurudumu manne(wheel chairs) kwa wagonjwa wanaohitaji msaada wa mtu mwingine ili kuwafikia watoa huduma.

Akipokea vifaa hivyo,muuguzi wa zahanati ya Njema Upendo Bora,amelishukuru Kanisa hilo kwa msaada huo kwani vifaa hivyo vitakwenda kuchochea uwajibikaji kwa watumishi na kutoa huduma bora kwa wagonjwa wanaofika kupata huduma za afya.

Alisema,vifaa hivyo vimetolewa kwa muda muafaka kwani kumekuwa na ongezeko kubwa la watu wanaofika katika kijiji hicho  kwa ajili ya shughuli mbalimbali wakiwemo wanunuzi wa mazao na wafugaji ambao watahitaji  kupata matibabu.

Mwenyekiti wa Serikali ya kijiji cha Njenga John Mtanga alisema,msaada wa vifaa tiba vilivyotolewa na kanisa hilo vitapunguza kero ya mama wajawazito wanaosubiri kujifungua au waliojifungua kulala zaidi ya mtu mmoja katika kitanda kimoja.

Kwa upande wake Askofu wa Kanisa la Upendo wa Kristo Masihi Noel Mbawala alisema,kanisa kupitia taasisi yake ya Kiuma imelazimika kutoa vifaa hivyo ili vitumike kuimarisha afya za watu kwa kutambua kuwa ili watu waweze kumjua Mungu na kushiri kwenye shughuli za maendeleo ni lazima wawe na afya njema.

Aidha alisema,kanisa limetoa vifaa tiba katika zahanati hiyo kutokana na mahitaji makubwa ya vifaa kwa ajili ya wagonjwa na kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Serikali ya awamu ya sita za kuimarisha na kuboresha huduma za afya katika wilaya ya Tunduru.

Askofu Mbawala,ameipongeza serikali  ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa jithada zake katika kuimarisha huduma za afya,maji,umeme na miundombinu ya Barabara ambayo imewezesha kuboresha na kuimarisha maisha ya Watanzania.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.