• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

KAZI ya kuunganisha lami ndani ya Wilaya inasonga mbele Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: April 20th, 2025

barabara ya kisasa ya lami kutoka Kitai, kupitia Ruanda hadi Bandari ya Ndumbi imeanza kuandikwa katika sura mpya ya maendeleo ya kusini mwa Tanzania.

Huu si mradi wa kawaida wa ujenzi wa barabara; ni dira ya matumaini kwa maelfu ya wananchi wanaoishi na kutegemea ukanda huu wa kimkakati.

Mradi huu unaolenga kujenga barabara yenye urefu wa kilomita 95, ni sehemu ya ajenda ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuboresha miundombinu ya usafiri ili kuunganisha kwa urahisi maeneo ya ndani na bandari za Ziwa Nyasa, na hivyo kufungua milango ya uchumi, biashara, na utalii katika Mkoa wa Ruvuma.


Bilioni 155  kutekeleza mradi huu

Kwa gharama ya takriban shilingi bilioni 155, Serikali imeweka mkazo mkubwa si tu katika kujenga barabara, bali katika kujenga maisha mapya kwa wananchi.

Mkandarasi aliyeteuliwa, kampuni ya China Railway Seventh Group (CRSG), anaendelea na kazi, akitekeleza mradi huu kwa awamu mbili ,awamu ya kwanza kutoka Amanimakolo hadi Ruanda yenye urefu wa kilomita 35, na awamu ya pili kutoka Ruanda hadi Bandari ya Ndumbi yenye urefu wa kilomita 50.

Tayari, kufikia Machi 2025,TANROADS Mkoa wa Ruvuma imeanza rasmi ujenzi wa awamu ya pili.


Barabara Inayoleta Maisha

Kwa wakulima wa kahawa, mahindi, na mazao mengine ya biashara kutoka Mbinga, barabara hii inamaanisha soko la haraka. Kwa wavuvi na wafanyabiashara wa Ndumbi, ni tumaini la mzunguko wa bidhaa na wateja.

Kwa wajasiriamali wa utalii, ni fursa mpya ya kuibua vivutio vilivyofichika vya Ziwa Nyasa.

“Hii barabara itatusaidia kusafirisha mazao yetu kwa haraka hadi bandarini, na hata kuyapeleka nje ya nchi,” anasema Mama Anna Mlagha, mkulima kutoka kijiji cha Ruanda.

Zaidi ya hayo, barabara hii inaunganisha Bandari ya Ndumbi na Bandari ya Mbambabay kiunganishi cha usafiri wa majini ambacho sasa kitapata nguvu mpya, na hivyo kuchochea shughuli za kibiashara kati ya Tanzania na nchi jirani  za Malawi na Msumbiji.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.