• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

KIGONSERA:Sekondari pekee nchini iliyotoa Rais na Waziri Mkuu

Imewekwa kuanzia tarehe: July 10th, 2020

SHULE ya sekondari ya Kigonsera iliyopo wilayani Mbinga mkoani Ruvuma ina historia ya kipekee hapa nchini kwa sababu ndiyo sekondari iliyoweza kuwatoa viongozi wawili wa ngazi ya juu kabisa nchini.

Ponsiano Ngungulu ni Mkuu wa sekondari  ya Kigonsera anasema shule hiyo ilianzishwa mwaka 1938 ikiwa ni seminari ya kanisa katoliki chini ya  Shrika la Wabenedikitini(Benedictine fathers) wa Peramiho hadi mwaka 1961 ilipochukuliwa na serikali.

Ngungulu anasema shule hiyo ya wavulana pekee, ina uwezo wa kuwahudumia wanafunzi 280 na kwamba tangu kuanzishwa kwake hadi sasa,shule hiyo imeweza kutoa jumla ya wahitimu 13,266.

“Shule wakati inaanzishwa na wakoloni ilikuwa na lengo la kutoa elimu ya  dini ya kikristo hususani dhehebu la kanisa katoliki hivyo baada ya uhuru serikali iliamua kuitaifish ili iweze kuwahudumia watanzania wote bila ubaguzi wa kidini’’,anasema.

Hata hivyo anasema tangu mwaka 1961 hadi mwaka 2011 sekondari ya Kigonsera imekuwa inatoa elimu ya sekondari kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza hadi cha nne na kuanzia mwaka 1998 hadi sasa sekondari hiyo imekuwa inatoa elimu ya kidato cha sita.

Sekondari ya Kigonsera imepata umaarufu mkubwa hapa nchini kwa sababu imeweka historia iliyotukuka baada ya viongozi maarufu wa kitaifa kusoma katika sekondari hiyo.

Mkuu wa sekondari ya Kigonsera anamtaja mmoja wa viongozi hao kuwa  ni Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Benjamin Mkapa ambaye alisoma  Kigonsera toka mwaka 1952 hadi 1953 kisha alihamia Ndanda mkoani Mtwara.

Ngungulu anamtaja Kiongozi mwingine wa kitaifa ambaye amesoma Kigonsera ni Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa ambaye alianza kidato cha kwanza na kuhitimu kidato cha nne katika sekondari hiyo mwaka 1980.

Licha ya viongozi hao sekondari ya Kigonsera imetoa viongozi wengine wengi  hapa nchini ,miongoni mwao ni  Dkt Modestus Kipilimba ambaye ni Balozi wa Tanzania nchini Msumbiji,Profesa Simon Mbilinyi aliyewahi kuwa Waziri wa Fedha na Mbunge wa Peramiho na Juma Homera Mkuu wa Mkoa wa Katavi.

Viongozi wengine waliosoma Kigonsera ni  Katibu Mkuu Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa  Dkt Frolens Turuka,Hayati Askofu Mstaafu wa Jimbo la Mbinga Imanuel Mapunda,Hayati Askofu Mstaafu wa Jimbo la Njombe Raymund Mwanyika ,Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu la Songea Norbeth Mtega,Askofu wa Jimbo la Lindi Mhashamu Bruno Ngonyani ,Askofu wa Jimbo la Mtwara Mhashamu Gabriel Mmole na  Askofu wa Jimbo la Njombe Mhashamu Alfred Maluma .

Moto wa shule ya sekondari ya Kigonsera, Elimu ni ukombozi na dira ya shule ni kutoa elimu bora ya kupambana na  changamoto mbalimbali  zinazotokana na mabadiliko ya Dunia.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari wa Mkoa wa Ruvuma

Julai 10,2020

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.