• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

KITUO cha Afya Mkasale kilivyofanikiwa kuwafanyia upasuaji kwa mafanikio wagonjwa 51

Imewekwa kuanzia tarehe: July 3rd, 2020

KITUO cha Afya Mkasale Kata ya Namasakata Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma kimeanza kutoa huduma za upasuaji ambapo hadi sasa watu 51 wamefanikiwa kufanyiwa upasuaji.

Akitoa taarifa ya kituo hicho kwa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Ruvuma,Mganga Mkuu wa kituo hicho Dr.Joseph Morris amesema kati ya watu waliofanyiwa upasuaji akinamama wajawazito ni 32 na wengine wasiokuwa wajawazito 19 na kwamba upasuaji kwa wote umefanyika kwa mafanikio makubwa.

Dr.Morisi amesema huduma ya upasuaji imeanza kutolewa katika kituo hicho tangu Machi mwaka huu ambapo idadi ya wagonjwa wanaohitaji huduma imekuwa inaongezeka na kwamba kituo  kina uwezo wa kulaza wagonjwa 36 ambapo kwa siku wanapokea wagonjwa 60.

Amesema kituo hicho kinazungukwa na zahanati nane ambazo zinakitegemea kituo hicho katika huduma mbalimbali za afya na kwamba kituo pia kinahudumia watu kutoka tarafa ya Nakapanya na Tunduru mjini.

“Kituo hiki kilianzishwa mwaka 1989,ukarabati umefanyika kuanzia mwaka 2018 baada ya serikali kutoa kiasi cha shilingi milioni 400 na kazi ya upasuaji imeanza mwaka huu kwa ufanisi mkubwa’’.alisisitiza.

Naye Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Ruvuma Odo Mwisho amesema serikali ya CCM imefanyakazi kubwa ya kuwaondolea kero wananchi wa Kata ya Namasakata baada ya kuanza kutoa huduma za upasuaji katika kituo hicho cha afya.

‘’Hakuna aliyetegemea kituo hiki cha afya kingeweza kutoa huduma za upasuaji  na  wagonjwa wote waliofanyiwa upasuaji wametoka salama ,haya ni mafanikio makubwa sana,kwa sababu kabla ya kuwepo kituo hiki wazazi wengi wamepoteza maisha kwa kusafiri umbali mrefu kutafuta huduma’’,alisisitiza Mwisho.

Wananchi wa kijiji cha Mkasale wameishukuru serikali kwa kufanikisha ujenzi wa kituo hicho ambacho wamesema kimekuwa mkombozi kwa wananchi wote na kupunguza vifo  ambavyo vilikuwa vinatokea kwa kukosa huduma jirani.

Kituo cha afya Mkasale baada ya kiufanyiwa ukarabati kinatoa huduma za wagonjwa wa nje,maabara,upasuaji,wodi ya wanaume,wodi ya wanawake,jengo la mama na mtoto na chumba cha kuhifadhia maiti.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Julai 2,2020

Tunduru

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.