• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

KIWANDA cha Kahawa Mbinga chakoboa kahawa tani zaidi ya 18,000 kutoka kwa walima

Imewekwa kuanzia tarehe: June 29th, 2023

KIWANDA cha Wakulima wa zao la kahawa wilaya ya Mbinga(MCCCO),katika msimu wa mwaka 2022/2023 kimepokea na kukoboa zaidi ya tani 18,875 za kahawa kavu kutoka kwa vyama vya msingi vya Ushirika(Amcos).

Meneja Mkuu wa Kiwanda hicho Festo Chang’a alisema hayo ,wakati akizungumza  ofisini kwake mjini Mbinga, kuhusiana na mafanikio ya kiwanda hicho chenye mchango mkubwa kiuchumi kwa wakulima na wilaya ya Mbinga.

Chang’a alisema,kiasi hicho ni kidogo ikilinganisha na uwezo wake wa kukoboa zaidi ya tani 35,000 kwa mwaka na hali hiyo imetokana na baadhi ya wakulima kutotambua kwamba kiwanda hicho ni mali yao na  wanapaswa kupeleka kahawa kwa wingi.

Alisema,kwa kuwa kiwanda hicho kinakabiliwa na ushindani kutoka kwenye viwanda vingine,ni wajibu wa wakulima kupitia Amcos zao kuhakikisha wanapeleka kahawa katika kiwanda chao ambacho  wana hisa nacho ili kuongeza mapato ya ushirika.

Aidha alisema,wanapopeleka kahawa wakulima watapata fursa zinazotolewa katika kiwanda hicho ikiwemo kuongeza nguvu wakati wa kuhudumia mashamba ya zao hilo  ikiwa shambani ili kupata kahawa bora.

Chang’a alisema,kiwanda hicho ni  muhimu  kwani Kwa muda mrefu kinachangia shughuli za maendeleo katika vijiji mbalimbali ambavyo Amcos zao zinapeleka kahawa  ikiwemo saruji,bati kwa ajili ya ujenzi wa shule,zahanati na miradi mingine ya maendeleo.

Alisema,kiwanda kinatoa ajira za muda na kudumu kwa baadhi ya wananchi wa Mbinga na wilaya  ya jirani ya Nyasa na Songea ambapo vijana wa kike na kiume hupata ajira ambazo zinawawezesha kujipatia kipato kwa ajili ya familia zao.

Kwa mujibu wa Chang’a ni kuwa,kama Amcos hazipeleki kahawa kwa wingi katika kiwanda hicho basi husababisha kuwepo kwa upungufu mkubwa wa ajira hasa kwa akina mama ambao hawawezi kufanya kazi ngumu.

Hata hivyo alisema, katika msimu wa mwaka 2023/2024 wamejipanga kuhakikisha kiwanda hicho kikongwe wilayani Mbinga,kinapata kahawa  nyingi kutoka kwa vyama vya msingi na vikundi mbalimbali vya wakulima vinavyojishughulisha na uzalishaji wa kahawa.

Afisa masoko wa kiwanda hicho David Haule alisema,kiwanda cha MCCCO kinasindika kahawa inayolimwa Mbinga ambayo ina ubora mkubwa na safi kwa matumizi ya kunywa na kuhamasisha wakulima na wananchi kunywa kahawa wanayolima wenyewe.

Haule alisema,sehemu kubwa ya kahawa inayosindikwa na kiwanda hicho usafirishwa nje ya mkoa wa Ruvuma kama vile Dar es slaam,Lindi,Mtwara,Dodoma,Iringa,Tanga na Mbeya kwa ajili ya kuuzwa.

Aliongeza kuwa,kahawa inayosindikwa katika kiwanda hicho imepata sifa kubwa kutokana na kuwa na radha nzuri na ndiyo inayopendwa zaidi Ulimwenguni kote ikilinganishwa na kahawa inayosindikwa katika viwanda vingine hapa nchini.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.