• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

KIWANJA cha Ndege Songea kubeba ndege kubwa sita kwa wakati mmoja,sasa ndege kutua saa 24

Imewekwa kuanzia tarehe: October 21st, 2020

SERIKALI  ya awamu ya tano imetenga  kiasi cha shilingi bilioni 37 kukarabati uwanja wa ndege wa Songea ambao utawezesha kwa wakati mmoja kubeba ndege sita aina ya bombardier.

Akitoa taarifa ya ukarabati wa kiwanja hicho kwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme,Meneja wa Uwanja wa Ndege wa Songea Jordan Mchami,amesema kazi ya  ujenzi wa barabara ya kutua ndege yenye urefu wa  meta 1740 na upana wa meta 30 imeshakamilika.

Amesema ujenzi wa maegesho ya ndege yenye ukubwa wa meta 139 kwa 126 ipo kwenye hatua za mwisho kukamilika na inatarajia kukamilika katikati ya mwezi Novemba mwaka huu hivyo kumudu kuegesha ndege kubwa zaidi ya  sita.

Meneja huyo wa Kiwanja cha ndege Songea amesema pia yamejengwa maegesho maalum ya kuegesha ndege za dharura yenye ukubwa wa meta 70 kwa 40  na kwamba katika kiwanja hicho zimejengwa taa za kisasa za kuongozea ndege wakati wa usiku  hivyo kuwezesha ndege kutua saa 24 yaani usiku na mchana.

“Ndege aina ya bombardier sasa zitaanza kutua wakati wowote katika kiwanja cha ndege cha Songea,tunatarajia ndege ya kwanza itatua kabla ya mwisho wa mwezi huu Oktoba’’,alisema Mchami.

Amesema jengo jipya la abiria lenye uwezo wa kuchukua abiria 150 kwa wakati mmoja limejengwa na kukamilika katika uwanja wa ndege wa Songea  hali ambayo inaweza kumudu abiria wa ndege mbili za bombardier kwa wakati mmoja.

Amesema gharama za nauli katika ndege hizo za serikali zitakuwa chini ukilinganisha na ndege ndogo za watu binfasi ambazo nauli yake ni kati ya shilingi 500,000 hadi 600,000  hali ambayo wananchi wengi hawawezi kumudu.

Amesema ujio wa ndege ya bombardier utakuwa ni ukombozi kwa wananchi wa Mkoa wa Ruvuma kwa sababu wananchi watalipa shilingi 400,000 toka Songea hadi Dar es salaam, kwenda na kurudi.

Akizungumza mara baada ya kukagua ukarabati wa uwanja huo,Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme ameipongeza Kampuni ya CHICCO ambayo inakarabati kiwanja hicho,ambacho ukarabati wake unatarajia kukamilika kwa asilimia 100 Desemba mwaka huu.

Mndeme amesema kiwanja cha ndege  wa Songea ni rasilimali adimu inayoweza kusaidia kukuza uchumi wa mji wa Songea na Mkoa mzima wa Ruvuma hasa kukuza sekta ya utalii,baada ya kuanzishwa mpango mkakati wa kukuza utalii katika mkoa wa Ruvuma.

Kiwanja cha ndege wa Songea ni miongoni mwa viwanja  bora vya ndege Tanzania ambacho kilijengwa kati ya mwaka 1974 hadi 1980 na kiliwekewa lami hivyo kuwa na uwezo wa kutua ndege majira yote masika na kiangazi.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Oktoba 21,2020

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.