• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

KUELEKEA Uchaguzi Mkuu Mawakala wa vyama waonywa

Imewekwa kuanzia tarehe: October 23rd, 2020

MSIMAMIZI wa Uchaguzi wa Jimbo la Peramiho Simon Bulenganija ametoa onyo kwa mawakala wa vyama vya siasa waliokusudia kuvuruga Uchaguzi Mkuu mkono wa sheria hautawaacha salama.

Bulenganija ametoa onyo hilo kwa nyakati tofauti wakati akiwaapisha kiapo cha kutunza siri mawakala wa vyama vya siasa ambao wameteuliwa na vyama vyao katika Mji mdogo wa Peramiho na Kijiji cha Mpitimbi katika Jimbo la Peramiho Mkoani Ruvuma.

Amesema kwa wakala yeyoto atakayejitoa ufahamu kwa lengo la kuvuruga Uchaguzi Mkuu, Oktoba 28, 2020 iwe,wakati wa kupiga kura, kuhesabu kura,kujumlisha kura na kutangaza matokea mkono wa sheria hauta muacha salama kwa sababu zoezi la uchaguzi lipo kwa mujibu wa kanuni taratibu na sheria za Nchi.

“Lazima mpime vizuri  kazi ya kusimamia maslahi ya chama   lakini pia  umuhimu na ulazima wa kuzingatia  sheria,kanuni,taratibu na maelekezo ya Tume”,alisema Bulenganija.

Ametahadharisha kila wakala kutimiza jukumu alilopangiwa na kuacha kuingilia jukumu ambalo wakala hakupangiwa katika kipindi cha kupiga kura,kuhesabu kura  kujumlisha kura na kutangaza matokeo.  

Hata hivyo amesema vyama ambavyo havijawasilisha orodha ya majina ya mawakala wa vyama vyao katika Ofisi ya Msimamizi wa jimbo la Uchaguzi hawataruhiswa kusimamia uchaguzi  kwa mujibu  wa maelekezo ya Tume ya Uchaguzi.

Amesema katika jimbo hilo vyama viwili tu ambavyo vimetimiza sharti hilo ambavyo ni Chama cha Maendeleo na Demokrasia (CHADEMA) na Chama cha Mapinduzi (CCM).

Amewakumbusha wananchi   wote wenye sifa na vigezo kujitokeza kwa wingi kwenda katika vituo  walivyojiandikisha kwenda kupiga kura  siku ya Jumatano Oktoba 28,2020 ili ktimiza haki yao ya kikatiba ya  kuhakikisha kila mtu anapiga kura kwa uhuru. 

Amesema maandalizi yote ya zoezi la uchaguzi yanaenda vizuri na tayari Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeshafikisha vifaa kwa asilimia 98 ambavyo vinatakiwa katika kufanikisha zoezi hilo.

Kwa upande wake Msimamizi Msaidizi wa Jimbo la Uchaguzi la Peramiho  Kangese Masanja amesema mawakala ni kundi la watu muhimu katika kufanikisha zoezi la uchaguzi ,hivyo ni vema wakazingatia maelekezo yote yanayotolewa na Tume na kujiepusha na udanganyifu wawapo katika vituo vya kupigia kura.

Jimbo la Peramiho lina Kata 16,Vijiji 56,vituo vya kupigia kura 252 na jumla ya mawakala 509 waliapa kiapo cha kutunza siri  katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Oktoba 23,2020

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.