• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MAAFISA Elimu watu wazima Ruvuma waagizwa kusimamia madarasa ya Kisomo na SEQUIP

Imewekwa kuanzia tarehe: October 2nd, 2024

MAAFISA Elimu Watu Wazima katika Halmashauri zote mkoani Ruvuma  wameagizwa  kuhakikisha wanasimamia uwepo wa madarasa ya kisomo na SEQUIP  katika kila Kata.

Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas Ahmed katika  hotuba iliyosoma kwa niaba yake na Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma Mary Makondo katika kilele cha maadhimisho ya  Juma la Elimu kimkoa ambayo yamefanyika Mbambabay wilayani Nyasa.

 “Niwaombe wananchi kujiunga kwa wingi katika madarasa hayo kama ilivyo dhamira ya Rais wetu Dkt.Samia Suluhu Hassan  kuhakikisha kila kijana wa kike aliyekatisha masomo anarejeshwa shuleni’’,alisisitiza Kanali Abbas.

Kupitia maadhimisho hayo,Mkuu wa Mkoa amewaagiza wakurugenzi wote wa Halmashauri na maafisa Elimu Msingi na Sekondari wahakikishe kuwa  elimu ya watu wazima inatiliwa mkazo kwa kuweka mikakati mizuri ili iweze kutekelezwa kikamilifu.

Akitoa taarifa ya utekelezaji wa shughuli za elimu ya watu wazima na elimu nje ya mfumo rasmi kwenye maadhimisho hayo,Afisa elimu Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mwl.Mathias Tilia  amesema Mkoa kwa kushirikiana na Taasisi ya elimu Tanzania unatekeleza program kwa wasichana waliokatisha masomo ya sekondari ambapo hadi sasa jumla ya wanafunzi 228 wananufaika na mradi huo.

Tilia amesema Mkoa wa Ruvuma una jumla ya vituo  70 vya elimu ya msingi kwa Watoto walioikosa (MEMKWA) vyenye jumla ya wanafunzi 317 kati yao wavulana 231 na wasichana 186 na kwamba wanafunzi hao walikosa fursa ya kupata elimu katika mfumo rasmi kutokana na changamoto mbalimbali za kimaisha.

Ameongeza kuwa Mkoa wa Ruvuma una vituo vitano vya ufundi stadi ambavyo hutoa mafunzo kwa wanafunzi waliomaliza elimu ya msingi na sekondari  katika fani za useremala,ushoni,udobi na upishi na kwamba vituo hivyo vinawapa ujuzi wa stadi mbalimbali vijana ili kuwawezesha kukabiliana na changamoto za kimaisha.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Mheshimiwa Peres Magiri akizungumza kwenye maadhimisho hayo yenye kaulimbiu ya ujumuishi katika elimu bila ukomo kwa ujuzi,ustahimilivu,amani na maendeleo,amesisitiza  wananchi kuendelea kupata elimu  kupitia mfumo usiokuwa rasmi kwa kuwa elimu haina mwisho.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.