• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MAAFISA Tarafa Ruvuma wakabidhiwa pikipiki walizopewa na Rais Magufuli

Imewekwa kuanzia tarehe: May 11th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amekabidhi Pikipiki 20 kwa maafisa Tarafa wa Mkoa wa Ruvuma ikiwa ni  utekelezaji wa ahadi ya Rais Dkt.John Magufuli aliyoitoa Ikulu mwaka 2019 katika kikao cha maafisa tarafa wote nchini..

Akizungumza  kabla ya kukabidhi pikipiki hizo, Mndeme amemshukuru Rais kwa upendo ambao haujawahi kutokea tangu nchi yetu ipate Uhuru  kwa kiongozi wa juu wa Taifa kukaa kikao Ikulu na maafisa Tarafa wote nchini.

 Amelitaja lengo la kutoa pikipiki hizo ni kuhakikisha shughuli za maendeleo kwa maafisa tarafa zinafanyika kwa viwango vinavyotakiwa na kuona uchumi wa wananchi unaimarishwa ipaswavyo.

Amesema pikipiki hizo zinagawanywa katika wilaya zote tano za Mkoa wa Ruvuma ambapo wilaya songea imepata pikipiki nne, Mbinga tano,Nyasa mbili,Tunduru saba na  Namtumbo mbili.

 “Pikipiki hizi mnapewa kusaidia katika kurahisisha mawasiliano kati ya ngazi ya kata na Halmashauri kwa upande mmoja na Serikali Kuu na Serikali za Mitaa kwa upande mwingine,pikipiki hizi zitunzwe ili ziweze kudumu kwa muda mrefu’’,alisisitiza Mndeme.

Amewaagiza Maafisa Tarafa wafuatilie na kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika maeneo yao na kuhakikisha wanasimamia ulinzi na usalama katika kata zilizomo ndani ya Tarafa husika.

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma Steven Ndaki amesema pikipiki hizo zilizotolewa na Rais Dkt.John Magufuli ni utekelezaji wa ahadi yake aliyoitoa kwa maafisa hao walipokuwa Ikulu mjini Dar es salaam.

Akizungumza kwa niaba ya maafisa tarafa waliopata pikipiki hizo,Afisa Tarafa wa Songea mjini Mashariki Agustino Chazua  amempongeza Rais Dkt.John Magufuli kwa kutekeleza ahadi yake kwa maafisa tarafa.

Amesema hivi sasa pikipiki hizo zitawasadia kutekeleza majukumu yao kwa asilimia 100 ambapo watahakikisha wanakwenda kusikiliza kero mbalimbali kwa wananchi katika vijiji vyote .

Imeandaliwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Mei 11,2020

 

 

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.