• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MAAGIZO ya Kamati ya Bunge ya LAAC Madaba hayajatekelezwa

Imewekwa kuanzia tarehe: April 2nd, 2024

MAAGIZO yote sita yaliyotolewa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) Oktoba 2022 katika Halmashauri ya Madaba wilayani Songea mkoani Ruvuma hayajatekelezwa hadi sasa.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas Ahmed katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Mheshimiwa Kisale Makoli  kwenye  kikao cha kujadili utekelezaji wa maagizo ya Kamati ya LAAC kilichofanyika kwenye ukumbi wa Halmashauri ya Madaba.

Maagizo hayo ni Pamoja na Halmashauri kuweka mikakati ya kufanikisha ukusanyaji wa mapato ya ndani yasiyopungua sh.bilioni mbili,kulipa kodi ya zuio ya shilingi milioni 24.9 kwa TRA,kusimamia suala la fidia ya sh.milioni 229.8 inayotokana na kuvunjwa kwa mkataba na TBA,kukusanya sh.milioni 8.2 kutoka kwenye vikundi na kufunga mfumo wa GOT-HOMIS kwenye vituo vya kutolea huduma za afya.

Kanali Abbas amesema Kamati ya LAAC  ilitoa maagizo hayo sita ambayo yalipaswa kutekelezwa kikamilifu na Menejimenti ya Halmashauri hiyo.

“Hali ya utekelezaji hadi sasa hairidhishi kabisa,hakuna agizo hata moja ambalo limetekelezwa na kufungwa,pia mwenendo wa kushughulikia hoja na mapendekezo ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali CAG bado hauridhishi kabisa’’,alisisitiza Kanali Abbas.

Kutokana na hali hiyo Mkuu wa Mkoa amewaomba waheshimiwa madiwani kufuatilia kwa karibu na kuhakikisha hoja zote zinajibiwa ipasavyo na kuweka mikakati ya kuhakikisha hoja hizo hazijirudii tena.

Kanali Abbas amewataka wakuu wa Idara kushiriki ipasavyo katika kuandaa majibu ya hoja na utekelezaji wa mapendekezo ya CAG ambapo ameuagiza uongozi wa Halmashauri hiyo kuchukua  hatua mapema za kinidhamu kwa watumishi wanaozalisha hoja.

Katika Halmashauri hiyo hadi sasa kuna jumla ya hoja na mapendekezo 52 ambayo yanatakiwa kufanyiwa kazi ili yafungwe.

Awali  Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma Rehema Madenge akizungumza kwenye kikao hicho ameuagiza uongozi wa Halmashauri hiyo kuhakikisha wanajitahidi kujibu hoja  zote kwa wakati ,kwa usahihi na kushirikiana watendaji wote wa Halmashauri husika kujibu hoja.

Amesisitiza kuwa hoja hizo zinazalishwa na watumishi hivyo watumishi wenyewe wanatakiwa kujibu hoja zote kwa wakati kama ilivyoelekezwa ili Kwenda na muda uliopangwa.

Akizungumza kwa niaba ya waheshimiwa Madiwani,Naibu Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mheshimiwa Oraph Pilly amesema wamesikitishwa na taarifa ya kushindwa kutekeleza  kwa wakati maagizo yote sita ya LAAC katika Halmashauri hiyo.

Kutokana na hali hiyo waheshimiwa madiwani hao wamemwomba Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo  ifikapo Aprili 5 mwaka huu kufanya kikao maalum cha kuangalia nini kilisababisha kushindwa kutekelezwa  maagizo  ya LAAC kwa wakati.

Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mheshimiwa Teofanes Mlelwa ameridhia kufanyika kwa kikao hicho maalum ambapo amesisitiza kuwa amekosa amani kutokana na Halmashauri hiyo kushindwa kutekeleza maagizo hayo kwa wakati na kwamba amepokea maagizo yote  yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa na kuahidi kuyafanyia kazi.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma amefanya vikao vya kujadili utekelezaji wa maagizo ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa yaliyotolewa katika mwaka wa fedha wa 2021/2022  katika Halmashauri saba za Mkoa wa Ruvuma.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.