• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MADABA yatumia milioni 196 kujenga mabweni mawili

Imewekwa kuanzia tarehe: March 19th, 2021


JUMLA ya shilingi milioni 196 zimetolewa na serikali kutekeleza  miradi ya ujenzi katika  shule ya Sekondari Mahanje iliyopo Halmashauri ya Madaba Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma.

Afisa Elimu Sekondari wa Halmashauri hiyo Michael Hadu amesema kati ya fedha hizo shilingi milioni 150 zimetumika kwa kujenga mabweni mawili,milioni 40 zimejenga madarasa mawili na milioni 6.6 zimetumika kujenga matundu ya vyoo.

 Amesema mabweni hayo yana uwezo wa kulaza wanafunzi 160 kila moja hivyo kupunguza kero kwa wanafunzi wa kike ambao walikuwa wanasafiri kila siku kilometa 24 kwenda na kurudi kwenye makazi yao.

Hata hivyo  amesema Halmashauri  ya Madaba ina jumla ya shule nane za sekondari ikiwemo shule ya  sekondari Mahanje ambayo  imefanikiwa kujengewa mabweni mawili ikiwa na wanafunzi zaidi ya 526 wanaosoma kidato cha kwanza hadi cha nne.

“Tuliweka mikakati ya kuboresha miundombinu ya shule hiyo ikiwemo mabweni,maabara,madarasa,maktaba na vyoo  kwa kweli mabweni haya yamesaidia kupunguza mimba kwa wanafunzi na kuongeza ufaulu”,alisema Hadu.

Akizungumzia maendeleo ya taaluma katika Halmashauri hiyo,Hadu amesema kwa miaka miwili mfululizo 2019 na 2020,Halmashauri hiyo  imeshika nafazi ya kwanza kimkoa kati ya Halmashauri nane za Mkoa wa Ruvuma katika mtihani wa Taifa wa kidato cha nne.

 Kaimu Mkuu wa shule ya sekondari Mahanje Agastini Mikibalisi amesema ufaulu katika shule hiyo  umeongozeka na kuondoa alama ya sifuri ambapo mwaka 2018 shule hiyo ilishika nafasi ya 25 kati ya shule 75 za Mkoa wa Ruvuma,mwaka 2019 ilishika nafasi ya 35 kati ya shule 137 za Mkoa wa Ruvuma na  mwaka 2020 ilishika nafasi ya 24 kati ya shule 145 za Mkoa wa Ruvuma.

 Amesema mabweni hayo yameleta faida katika shule hiyo na kufikia idadi kubwa ya wanafunzi wanaohudhuria  masomo yao na kufanya vizuri katika mitihani yao.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Machi 19,2021

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.