• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MADIWANI Tunduru wamshukuru Rais Samia kwa fedha za miradi

Imewekwa kuanzia tarehe: September 5th, 2023

Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma wamefanya baraza la robo ya nne kwa mwaka wa fedha ulioishia juni 2023 tarehe 27/08/2023 katika ukumbi wa mikutano claster uliopo Tunduru.

Mkutano huo wa baraza ulihudhuriwa na Waheshimiwa Madiwani , Mkuu wa wilaya ya Tunduru ,Mkurugenzi mtendaji, Ofisi ya RAS ,Wakuu wa idara na vitengo na Maafisa tarafa.

Akizungumza, Mwenyekiti wa mkutano Mheshimiwa Hairu Mussa ambaye ni Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Tunduru , ameishukuru serikali ya awamu ya sita chini ya Mheshimiwa ,Dkt. Samia suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kazi kubwa ya kuendelea kuinua maendeleo katika wilaya ya Tunduru.

"Tunaishukuru serikali kwa kutuletea miradi mingi ambayo haijawahi tokea kwa kipindi cha nyuma". Alisema.

Aidha Mheshimiwa Hairu amewasisitiza wataalamu ,kuzidi kusimamia zoezi la ukusanyaji wa mapato kwa ukaribu ili kuongeza mapato, ambayo yanakwenda kukamilisha miradi yetu ya maendeleo iliyopo katika kata na vijiji.

Vile vile amesisitiza idara ya kilimo maafisa ugani kuwa na karibu na wakulima ,ili kuweza kuwasaidia mbinu bora za kuweza kuongeza uzalishaji, hasa katika mazao haya ya biashara katika wilaya yetu ya Tunduru.

Aidha, Mkuu wa wilaya ya Tunduru Mheshimiwa Julius Mtatiro, amesisitiza katika kuongeza vyanzo vya mapato katika Halmashauri ya wilaya ya Tunduru , na kuangalia fursa mpya zitakazoweza kuongeza ukusanyaji mapato katika Halmashauri ya wilaya ya Tunduru.

Vile vile Mhe. Mtatiro amewataka madiwani kusimamia kwa ukaribu suala la ufugaji holela wakishirikiana na watendaji wao wa maeneo hayo, ikiwa ni pamoja na kuwahimiza wananchi kutouza maeneo yao yanayosababisha kukaribisha ufugaji holela katika wilaya yetu.

"Ninyi ni wawakilishi wa wananchi katika maeneo yenu,tukaongeze nguvu ya mikutano na watendaji wetu, tusaidiane kusimamia ili kuondoa ufugaji holela " alisisitiza Mhe. Julius Mtatiro.

Baraza la madiwani liliambatana na uchaguzi wa viongozi ngazi kuu tatu,kamati ya maadili ambayo itaongozwa na Mh. Hamisi Kaesa Diwani wa kata ya Matemanga, kamati ya Uchumi itaongozwa na Mh. Ado Saidi Tima Diwani kata ya Mchesi, na kamati ya huduma za jamii itaongozwa na Mh. Stawa Timamu Diwani viti maalumu kata ya Matemanga.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.