• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MAKAA ya mawe Ruvuma yaingiza Dola za Marekani zaidi ya milioni 144.9

Imewekwa kuanzia tarehe: March 26th, 2024

Na Albano Midelo,Songea

UZALISHAJI wa madini ya makaa ya mawe katika Mkoa wa Ruvuma  umekuwa chanzo kikubwa cha mapato ya serikali ambapo katika mwaka wa fedha wa 2023/2024,serikali imeweza kuuza tani 1,356,249.84 za makaa ya mawe zenye thamani ya Dola za Marekani Zaidi ya milioni 144.9.

Kwa mujibu wa taarifa ya Afisa Madini Mkazi  Mkoa wa Ruvuma,kiasi hicho cha madini kimeuzwa katika kipindi cha kuanzia Julai hadi Septemba 2023 pekee.

Kupitia mauzo hayo serikali imekusanya kiwango cha mrabaha wa Dola za Marekani 3,937,434.98 na ada ya ukaguzi Dola za Marekani 914,034.68 na kwamba madini hayo yameuzwa ndani ya nchi,nchi Jirani,barani Ulaya na Asia kupitia bandari ya Mtwara na Dar es salaam.

Hata hivyo Ofisi ya Afisa Madini Mkazi  Mkoa wa Ruvuma katika kipindi cha mwaka wa fedha 2023/2024 ilipangiwa kukusanya jumla ya shilingi  bilioni 41 na kwamba katika kipindi cha kuanzia Julai hadi Desemba ofisi hiyo ilikusanya Zaidi ya shilingi  bilioni 13  sawa na asilimia 64.

Uchimbaji na uuzaji wa makaa ya mawe mkoani Ruvuma ulianza mwaka 2011 kukiwa na Kampuni moja ya uchimbaji ya Tancoal Energy ambapo hadi kufikia mwka 2019  wadau wengi walijitokeza na kufanya uwekezaji  mkubwa katika uzalishaji wa  madini ya makaa ya mawe.

Kwa mujibu wa taarifa ya Afisa Madini  Mkazi,kwa kipindi cha  miaka mitano iliyopita,Mkoa wa Ruvuma umeweza kupata wawekezaji wengi   katika uchimbaji,ununuzi na uchenjuaji madini ya makaa ya mawe.

Ameutaja mchango wa sekta ya madini mkoani Ruvuma kuwa ni Pamoja  kutoa ajira kwa mtu mmoja mmoja na kupunguza utegemezi,kuongeza fedha za kigeni kutokana na mauzo ya madini nje ya nchi na kuongeza mapato ya Halmashauri yatokanayo na ushuru wa huduma.

Hata hivyo taarifa hiyo imezitaja changamoto za sekta ya madini mkoani Ruvuma kuwa ni Pamoja na uharibifu wa mazingira kutokana na kukata miti na kuchafua vyanzo vya maji,ubovu wa barabara ya kutoka migodini na changamoto ya upimaji wa  viwango vya ubora wa madini ya makaa ya mawe.

Changamoto nyingine ni kukosekana kwa teknolojia ya kisasa ya kuongeza ubora wa makaa ya mawe ili kushindana na soko,uwepo wa leseni za utafiti na uchimbaji ambazo haziendelezwi,uelewa mdogo wa taarifa za kijiolojia,utambuzi wa aina za madini,thamani yake na masoko ya madini jambo linalosababisha kusimama kwa uzalishaji wa madini ya shaba katika eneo la Mbesa wilayani Tunduru.

Ameitaja Mikakati ya kukabiliana na changamoto hizo kuwa ni kuendelea kuhamasisha wachimbaji wa makaa ya mawe na wawekezaji wengine kuleta mitambo ya kuosha madini ili kuongeza ubora,kusimamia kurudishwa kwa shughuli  mgodi wa Tancoal Energy na kuendelea kutoa elimuya sheria ya madini.

Ofisi ya Madini Mkoa wa Ruvuma pia inasimamia  masoko mawili ya madini ya dhahabu na vito yaliyopo wilayani Songea na Tunduru.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.