• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MAKANISA ya kipentekoste Ruvuma yatoa msaada wa vifaa vya corona

Imewekwa kuanzia tarehe: June 4th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amepokea msaada wa Vifaa vya kupambana na Corona vyenye thamani ya sh.  milioni  1.5 kutoka Baraza la Makanisa ya Kipentekoste Tanzania (CPCT) Mkoa wa Ruvuma.

Hafla  ya kukabidhi vifaa hivyo imefanyika leo katika viwanja vya ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma mjini Songea na kuwashirikisha viongozi mbalimbali wa  CPCT.

Mndeme amelishukuru Baraza la CPCT Mkoa wa Ruvuma kwa msaada huo ambao amesema tangu Ugonjwa huo uingie mkoani Ruvuma,ni mara ya kwanza kupokea msaada kutoka kwenye madhehebu ya Dini.

Hata hivyo Mndeme amewaomba Viongozi wa Dini  kuendelea kumuomba Mungu na Kumshukuru kwa Neema zake ili Taifa la Tanzania liendelee kuwa salama dhidi ya corona.

Mndeme amesema hadi kufikia Mei 4,mwaka huu katika  Mkoa wa Ruvuma kwenye vituo nane vya kulaza wagonjwa wa corona, hakuna Mgonjwa hata  mmoja na kwamba Mkoa upo salama ambapo ametoa rai kwa viongozi wa dini kuendelea kufanya maombi ili ugonjwa huo uweze kutokomezwa nchini na duniani kote.

 ‘’Mimi niendelee kuwaomba sana viongozi wa dini, kwa majitoleo yenu kwa watanzania, na  kuliombea Taifa Letu na Rais wetu anaendelea kutuhimiza kuchukua Tahadhari,na mimi nachukua fursa hii kuwaahidi  vifaa hivi vitatumika  kwa malengo kusudiwa’’. Alisema

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Umoja wa Makanisa ya Kipentekoste Mkoa wa Ruvuma Mchungaji Andrew Kyando amevitaja vifaa ambavyo CPCT wamevitoa kuwa ni ndoo kumi za kunawia mikono na sabuni za maji 30.

Vifaa vingine ni mashine tano za kunawa  maji ambazo zinatumika bila kugusa kwa ajili ya usalama zaidi,kipima joto la mwili kimoja(Thermal scanner) ambapo amesema vifaa vyote vimegharimu shilingi milioni 1.5.

Amesema CPTC inaunga mkono juhudi za serikali katika vita ya corona na kwamba inatambua umuhimu wa kutoa msaada huo ili wananchi wa Mkoa wa Ruvuma waendelee kujikinga na  wawe salama dhidi ya maambukizi ya virusi vya corona.

Naye Katibu wa Baraza la CPCT  Mchungaji Elimu Mwenzegule amemchukuru Mkuu wa  Mkoa wa Ruvuma  kwa kuwashirikisha Maaskofu,Wachungaji tangu ulipoingia ugonjwa hatari wa Corona Nchini.

Mchungaji Mwenzegule  amesema anamshukuru Mungu kwa kusikiliza maombi ya watanzania ambapo hivi sasa maambukizi ya corona nchini yamepungua kwa kiasi kikubwa.

Baraza la makanisa ya kipentekoste Tanzania linajumuisha umoja wa makanisa ya kilokole zaidi ya  80 yalipo nchini.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari wa Mkoa wa Ruvuma

Juni 4,2020

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.