• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MAMLAKA ya maji safi mjini Mbinga ilivyofanikiwa kusambaza maji kwa wananchi wa pembezoni

Imewekwa kuanzia tarehe: March 17th, 2023

MAMLAKA ya maji safi na usafi wa mazingira Mbinga mjini(Mbiuwasa),imefanikiwa kusambaza huduma ya maji safi na salama kwa wakazi wa mji wa Mbinga na maeneo ya pembezoni kwa asilimia 79.2.

Mkurugenzi Mtendaji wa Mbiuwasa Mhandisi Yonas Ndomba alisema hayo  jana,wakati akieleza utekelezaji wa shughuli  mbalimbali na mafanikio ya mamlaka hiyo katika kipindi cha miaka miwili ya uongozi wa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.

Alisema kabla ya Rais Dkt Samia Hassan kuingia madarakani,Mbiuwasa ilikuwa na uwezo wa kusambaza huduma ya maji  kwa asilimia 52.5 tu katika kata tano,lakini sasa eneo linalopata huduma ya maji safi na salama limeongezeka hadi kufikia kata 8.

Ameongeza kuwa,idadi ya wateja waliounganishiwa huduma ya maji safi na salama imeongezeka kutoka 2,900 mwaka 2021  hadi 4,332 kufikia mwezi Disemba mwaka 2023.

Ndomba alitaja mafanikio mengine ni kuongeza mtandao wa maji,kufunga dira(mita)kwa wateja wote,kuongeza ubora wa maji na kuwajengea uwezo watumishi wake ili waweze kutekeleza majukumu yao ipasavyo.

Kwa mujibu wa Ndomba,mafanikio hayo kwa  Mbiuwasa yamepatikana baada ya serikali kupitia wizara ya maji kutoa zaidi ya shilingi bilioni 1.5 kwa mwaka wa fedha 2021/2022 zilizofanikisha kujenga mradi mkubwa wa maji wa Lusaka.

Alisema,kukamilika kwa mradi huo na mingine itakayotekelezwa katika maeneo mbalimbali,inalenga kuhakikisha huduma ya maji katika mji wa Mbinga inafika karibu na wananchi,kuchochea shughuli mbalimbali za maendeleo na kumtua mama ndoo kichwani.

Katika hatua nyingine Ndomba alisema,kwa mwaka wa fedha 2023/2024 wanatarajia kutekeleza mradi mkubwa wa maji utakao gharimu shilingi bilioni 4.6  fedha kutoka serikali kuu kwa ajili ya kuwezesha mji wa Mbinga kuwa na huduma ya maji safi na salama kwa asilimia 100.

Ndomba,amewaomba wakazi wa mji wa Mbinga kuanza kuingiza maji ndani ya nyumba zao

badala ya kutumia vituo maalum vya kuchotea maji(DPS) na kuwa walinzi wa miradi na miundombinu inayojengwa ili iweze kudumu kwa muda mrefu.

“sasa hivi tunaendelea na kampeni ya kuhamasisha wananchi kuhusiana na ujenzi wa vyoo bora ambavyo vinahitaji maji ya kutosha,kwa hiyo ni muhimu watu wavute maji kwenye nyumba zao”alisisitiza Ndomba.

Baadhi ya wakazi wa kata ya Betherehemu Halmashauri ya mji Mbinga,wamemshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha zilizofanikisha kujenga na kukamilika  kwa mradi wa maji wa Lusaka.

Wamesema,mradi huo umepunguza shida ya upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama na kuwaondolea usumbufu wa kuamka usiku wa manane kwenda kutafuta maji kwa ajili ya matumizi ya familia zao.

Diwani wa kata ya Betherehemu Ngonepo Amanyisye alisema huduma  ya maji safi na salama katika kata hiyo ilikuwa changamoto kubwa, lakini katika kipindi cha miaka miwili ya Serikali ya awamu ya sita kero hiyo imepungua kwa asilimia 85.

Alisema,hapo awali wananchi hasa wanawake wa kata ya Betherehemu ndiyo walikuwa waathirika wakubwa zaidi kwani walilazimika kuamka usiku wa manane kwenda kutafuta maji yaliyopatikana

kwenye visima vya asili na mabondeni licha ya maji hayo kutokuwa  safi na salama hasa wakati wa masika.

Alisema,mradi wa maji Lusaka umeleta mapinduzi makubwa ndani ya kata ya Betherehemu kwani sasa hakuna mwananchi anayekwenda mtoni kuchota maji au kutumia maji ya visima vya asili kwa matumizi yao ya kila siku.

Hata hivyo,ameiomba serikali kupitia wizara ya maji kuendelea kutenga fedha za kutosha kwa ajili ya kusambaza mtandao wa maji katika maeneo mbalimbali ili wananchi wapate huduma hiyo karibu na makazi yao.

Laurent Ngonyani mkazi wa Majengo alisema, siku za nyuma hali ya huduma ya maji haikuwa nzuri  ambapo wananchi  waliamua kuchimba visima vifupi na virefu kwenye makazi yao ili angalau wapate maji kwa ajili ya matumizi yao.Ameishauri Mbiuwasa,kuhakikisha inasogeza bomba kuu kwenye makazi yao ili kuwapunguzia wananchi gharama kubwa ya kuingiza maji katika nyumba zao.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.