• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MAZOEZI mawili ya uwekaji wazi na uboreshaji daftari la kudumu la wapigakura kufanyika Songea kwa siku tatu

Imewekwa kuanzia tarehe: May 1st, 2020

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) inafanya mazoezi mawili ya uwekaji wazi  na uboreshaji wa daftari la kudumu la Mpigakura  katika Jimbo la Uchaguzi la Songea mjini kuanzia Mei 2 hadi 4 mwaka huu.

NEC Jimbo la Songea mjini tayari imetoa mafunzo kwa kuzingatia miongozo ya kujikinga na virusi vya corona kwa waandishi wasaidizi na BVR KIT OPERATORS wapatao 42 watakaofanya kazi katika kata 21 za Manispaa ya Songea.

 Walioteuliwa kufanya kazi hiyo  wamekula kiapo na kupata Mafunzo ambayo yametolewa kwa siku moja kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea na kufunguliwa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Philipo Beno.

Akizungumza kabla ya kufungua mafunzo hayo,Beno amewatahadharisha wote walioteuliwa  kufanyakazi ya zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura awamu ya pili katika kata zote 21 za Manispaa hiyo kuchukua tahadhari kwa kujilinda  na kuwalinda wengine dhidi ya virusi vya corona.

“Kwa kuwa ninyi ndiyo wasimamizi hakikisheni kila anayekuja anaosha mikono kwa maji tiririka na sabuni na pia avae barakoa kwa sababu hivi sasa barakoa zipo  za kutosha,wewe utakuwa naye kwa karibu wakati mnafanya mahojiano kwa hiyo wewe utakuwa umejikinga na yeye atakuwa amejikinga’’,amesisitiza Beno.

Nuru Riwa ni Afisa wa Tume Idara ya Habari na Elimu ya Mpigakura  amesema Tume ya Uchaguzi imenunua vifaa vyote muhimu vya kujikinga na virusi vya corona vikiwemo barakoa,vitakasa mikono,ndoo za maji,sabuni,mipira ya kuvaa mikononi na sipiriti ambapo amewaasa walioteuliwa kufanyakazi hiyo kuhakikisha wanavitumia ipasavyo vifaa ili kujikinga na corona wakati wanatekeleza majukumu yao.

“Utakapokuwa vituoni ili usichukue wala kusambaza virusi vya corona ni lazima ujikinge,tumia vifaa vyote ulivyopewa kwa sababu corona ni hatari,lengo ni kwamba unapomaliza ili zoezi usipokee maambukizi wala kuwaambukiza wengine’’,alisisitiza Riwa.

Amesema zoezi hilo katika Manispaa  ya Songea linatarajia kufanyika kwa siku tatu kuanzia Mei 2 hadi 4,2020 na kwamba yanafanyika mazoezi mawili  ambayo ni uwekaji wazi wa daftari la kudumu la mpigakura na uboreshaji wa daftari la kudumu  la wapiga kura.

Kwa mujibu wa Afisa huyo, zoezi hilo japo linatumia siku tatu ni zito kwa sababu linafanyika katika mwaka wa uchaguzi Mkuu na kwamba mazoezi haya kabla ya uchaguzi yanafanyika Tanzania bara ya visiwani.

Ameitaja mikoa inayohusika katika mazoezi hayo kwa upande wa  Tanzania bara kuwa ni Ruvuma, Njombe, Lindi, Mtwara, Dodoma,Singida,Rukwa,Mbeya,Morogoro,Iringa,Dar es salaam na Pwani na kwamba Tanzania visiwa ni ni Unguja na Pemba.

“Katika mazoezi haya ya uwekaji wazi daftari la wapigakura na uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura kwa awamu ya pili tunaanza tarehe 2/5/2020 hadi 4/5/2020,tunaomba wananchi kujitokeza ili kuhakiki taarifa zake,orodha ya  majina ya wapigakura itabandikwa kila kituo’’,alisema.

Hata hivyo ametoa rai kwa wananchi  wanapofika kwenye vituo hivyo kuzingatia tahadhari za afya dhidi ya virusi vya corona na kwamba inashauriwa katika familia moja kumchagua mtu mmoja kuhakiki taarifa za wengine ili kuepukana na mkusanyiko ambao ni hatari kuambukizwa na corona.

Adamu Mkina ni Mkurugenzi Msaidizi wa Mipango,Tume ya Taifa ya Uchaguzi,Idara ya Mipango,Ufuatiliaji na Tathmini  amesema katika zoezi hilo mfumo utafunguliwa ndani ya kata  husika.

Ametoa rai  kwa wananchi watakaokuwa wanafika kuhakikiwa katika zoezi hilo kujua Mtaa au kijiji anachotoka ili kuwarahisishia walioteliuwa kufanya kazi hiyo ya kitaifa.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Aprili 30,2020

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.