• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MBIFACU kukarabati hoteli ya MBICU katika viwango vya kimataifa

Imewekwa kuanzia tarehe: July 5th, 2020

HOTELI YA MBICU MBINGA KUWA NA HADHI YA KIMATAIFA

CHAMA Kikuu cha Ushirika Wilaya ya Mbinga Nyasa (MBIFACU) mkoani Ruvuma kimeanza  mradi wa ukarabati wa  hoteli ya MBICU ambayo inamilikiwa na chama hicho ili iweze kuwa na  viwango vya kimataifa.

Kaimu Meneja wa MBIFACU Henrick Ndimbo  amesema ukarabati wa hoteli hiyo ambao umeanza mwaka wa fedha wa 2019/2020 unatarajia kukamilika baada ya miaka mitatu na kwamba katika kutekeleza mradi huo zaidi ya shilingi bilioni moja zitatumika.

Hata hivyo amesema ukarabati wa hoteli hiyo unafanyika kwa awamu ambapo katika awamu ya kwanza yanajengwa majengo sita na kujenga uzio ambao utazunguka eneo lote la hoteli hiyo.

“Eneo hili litakuwa majengo 15 pamoja na jengo la hoteli,majengo yote yataezuliwa na kuezekwa katika mtindo wa kisasa  ili kukidhi viwango vya kimataifa na kuvutia wageni wa ndani na nje ya nchi’’,alisisitiza  Ndimbo.

Kwa upande wake Kaimu Mwenyekiti wa MBIFACU Winfred Lupembe amesema mara baada ya kukamilisha mradi huo wanatarajia kuongeza mapato makubwa kupitia hoteli ya MBICU ambayo wageni watakuwa wanapata malazi, chakula na hudumu nyingine.

Henrick Ndimbo/Kaimu Meneja MBIFACU

Amesema kutokana na hoteli hiyo kuwa na hadhi ya kimataifa wanatarajia kupokea wageni wa kimkoa,kitaifa na kimataifa na kwamba  Bodi ya chama hicho imefanikiwa  kusimamia shughuli za ukarabati wa hoteli hiyo ambazo zinaendelea vizuri na wanatarajia kukamilisha kwa wakati.

Bumi Masuba ni Mrajisi Msaidizi wa Vyama vya Ushirika mkoani Ruvuma anasema kuwa hoteli ya MBICU ilijengwa miaka ya 1990 na kwamba ilisimama kutoa huduma kutokana na ubovu wa miundombinu yake.

Hata hivyo amesema MBIFACU wameamua kuifanyia ukarabati mkubwa hoteli hiyo  na mara baada ya ukarabati kukamilika hoteli ya MBICU itakuwa ni miongoni mwa hoteli bora zaidi katika Mkoa wa Ruvuma.

“Hoteli hii itakuwa ni ya kipekee katika Mkoa wa Ruvuma kwa sababu mgeni atapata mahali pa kulala,kula,kunywa,bustani maarufu ya kupumzikia,eneo la kuegesha magari,hii ni hoteli yenye eneo kubwa sana ina kila kitu,hapa itakuwa ni zero grazing’’,alisisitiza Masuba.MBIFACU ni Chama cha Ushirika ambacho kilianzishwa Agosti mwaka 2000 na kinafanya shughuli zake katika wilaya za Mbinga na Nyasa,chama hicho pia kinatoa huduma kwa wakulima wanaolima kahawa wilaya ya Songea. songeamc.go.tz 

Picha chini ukarabati wa majengo mapya ya hoteli ya MBICU   

Imeandikwa na Albano Midelo

 

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

 

Julai 5,2020

 

Mbinga

 


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.