• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MBINGA yatoa kingatiba ya usubi kwa asilimia 80.4

Imewekwa kuanzia tarehe: August 21st, 2023

Mbinga. Katika kipindi cha siku tatu tuu Halmashauri ya Mji wa Mbinga imefikia asilimia 80.4 ya lengo la kuwapatia kinga tiba ya usubi wakazi 126,866 ndani ya siku saba.  

Usubi ni ugonjwa  unaoathiri ngozi na macho ambapo husababisha ngozi kuwasha sana na kuwa ngumu kama mamba, kenge au mjusi na yenye madoadoa kama chui na bila matibabu hupelekea upofu.

Vimelea vya ugonjwa huu huenezwa na nzi wadogo weusi wanaopatikana katika mito inayoenda kwa kasi.

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Mbinga Dkt Kung'e Nyamuryekung'e alisema waliopatiwa kinga tiba mpaka leo Agosti 19 ni watu 102,016.

Ili kusema zoezi la kinga tiba ya usubi limefanikiwa inatakiwa kumezesha dawa walau asilimia 80 ya wakazi wa Halmashauri ya Mji wa Mbinga kati ya Agosti 17 zoezi lilipoanza na Agosti 23 siku litakapotamatika.

Tafsiri ya kufikia asilimia 80.4 ya lengo siku ya tatu baada ya zoezi kuanza ni kwamba kuna uwezekano mkubwa Halmashauri ya Mji wa Mbinga ikafikia na hata kuzidi lengo kabla ya siku saba zilizopangwa kumalizika.  

"Zoezi linakwenda vizuri. Mwitiko wa wananchi ni mkubwa tofauti na miaka ya nyuma," alisema Dkt Nyamuryekung'e.Kwa muda mrefu usubi, ugonjwa maarufu kama River blindness, umekuwa moja ya magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele na umekuwa ukiathiri sana jamii.

Hiyo ni kwa mujibu wa Mratibu wa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele----Halmashauri ya Mji wa Mbinga, Bi Sheila Mbike

Alisema vimelea vya ugonjwa wa usubi huchelewa kujitokeza na kwamba inaweza kuchukua miaka mitano hadi 10.

"Ni vizuri kuchukua tahadhari kwani athari za ugonjwa huu ni kubwa---inaweza kupelekea upofu na hivyo kupunguza nguvu kazi," alisema Bi Sheila.

Kinga tiba ya usubi ni zoezi la kitaifa ambalo hufanyika kila mwaka chini ya Wizara ya Afya katika baadhi ya maeneo yenye maambukizi makubwa.

Kwa Halmashauri ya Mji wa Mbinga, zoezi hilo lilizunduliwa katika Kata ya Mbinga mjini B na Diwani wa kata hiyo Mh Sultan Andoya Alhamisi ya Agosti 17, 2023.


Ugonjwa wa usubi umekua pasua kichwa kwa muda mrefu si kwa Tanzania tuu, bali duniani kwote.  


Mnamo Desemba 2015, zaidi ya wajumbe 200 kutoka mataifa 23 barani Afrika pamoja na mashirika ya kimataifa walikutana jijini Kampala, Uganda kujadili mikakati ya kutokomeza ugonjwa wa usubi.

Mpaka kipindi hicho (2015), ugonjwa huo uliathiri watu milioni 120 katika mataifa 35 duniani.

Katika kipindi hicho, barani Afrika pekee angalau watu 800,000 kati ya milioni 31 walioathirika walipoteza uwezo wa kuona.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.