• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MBUNGE wa Namtumbo amshukuru Rais Samia kwa miradi

Imewekwa kuanzia tarehe: April 6th, 2025

Mbunge wa Jimbo la Namtumbo, mkoani Ruvuma Mheshimiwa Vita Kawawa, amemshukuru Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kutoa Shilingi bilioni 7.798 kuboresha huduma ya majisafi na salama katika Mji wa Namtumbo.

Kawawa amesema hayo wakati anazungumza kwenye mkutano wa hadhara na wananchi wilayani Namtumbo katika ziara ya Katibu Mkuu CCM Balozi Dkt Emanuel Nchimbi akieleza kuwa hatua hiyo imeleta afueni kubwa kwa wananchi.

Katika hotuba yake, Kawawa amepongeza pia uamuzi wa Serikali kuruhusu kuendelea kwa utafiti wa mradi wa madini ya Uran, akifafanua kuwa mradi huo utakapotekelezwa utakuwa chanzo cha mapato kwa Serikali na Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo.

“Ndani ya kipindi cha miaka minne, Wilaya ya Namtumbo imepokea fedha zilizowezesha ujenzi wa shule tano za sekondari, ikiwemo Shule ya Sekondari Dkt Samia Suluhu Hassan iliyogharimu zaidi ya Shilingi bilioni 4, na shule za Msisima na Hanga zilizogharimu Shilingi milioni 600 kila moja”,alisema Kawawa

Aidha, Kawawa amesema Serikali ya awamu ya sita imetoa zaidi ya Shilingi bilioni 6.147 kujenga zahanati mpya 15, vituo vya afya, pamoja na ununuzi wa dawa na vifaa tiba, hatua ambayo imesaidia kuboresha huduma za afya na kupunguza vifo vya mama na mtoto wilayani humo.

Mbunge huyo amemuomba Katibu Mkuu wa CCM Taifa kuikumbusha Serikali kuhusu ahadi ya ujenzi wa barabara za Mtwarapachani–Nalas–Tunduru Mjini na Lumecha–Hanga–Malinyi hadi Ifakara kwa kiwango cha lami, akisisitiza kuwa barabara hizo ni muhimu kwa maendeleo ya kiuchumi.

Kwa mujibu wa Kawawa, ujenzi wa barabara hizo utachochea uchumi kwa kuwa maeneo yanayopitiwa yanazalisha mazao mengi ya chakula na biashara ambayo yanahitaji masoko ya uhakika na usafirishaji wa uhakika.

 Kwa upande wake Katibu Mkuu wa CCM, Dkt Emanuel Nchimbi, amewataka Wakala wa Mbegu ASA kuongeza uzalishaji wa mbegu na kufungua ofisi wilayani Namtumbo ili wakulima wanufaike na juhudi za Serikali katika sekta ya kilimo.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.