• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MIKATABA huduma Jumuishi Kanda ya Kusini yasainiwa Songea

Imewekwa kuanzia tarehe: December 13th, 2024

MIKATABA ya utoaji huduma jumuishi za UKIMWI na kifua kikuu  kupitia mradi wa USAID Afya yangu Kanda ya Kusini katika kipindi cha mwaka 2024/2025 imesainiwa  mkoani Ruvuma.

 Hafla ya kusaini mikataba hiyo imeshirikisha wakurugenzi wa Halmashauri zote nane mkoani Ruvuma na kufanyika kwenye viwanja vya ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma mjini Songea ambapo mgeni rasmi aliikuwa ni Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma Ndugu Joel Mbewa.

Akizungumza kwenye hafla hiyo Mbewa amesema   Utekelezaji Wa Bajeti ya mwaka 2024/2025 kupitia Mradi wa USAID AFYA YANGU Kanda ya kusini kwa ngazi ya Mkoa, Halmashauri na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa, wanatekeleza  afua za UKIMWI,Kifua Kikuu na huduma jumuishi za uzazi wa Mpango na Jinsia.

“Katika kipindi cha mwaka 2024/2025 Serikali ya Marekani imetenga jumla ya fedha kiasi cha TZS.4,14,873,990.55 kwa ajili ya kusaidia shughuli za utoaji wa huduma za UKIMWI na Kifua Kikuu kupitia Mamlaka ya Mkoa, Halmashauri zote Vituo vya Mashirika ya Dini na Asasi ya kiraia ya ROA’’,alisema

 Amesema Serikali ya Marekani kupitia Mfuko wa Dharura wa Rais wa Marekani wa kukabiliana na UKIMWI (PEPFAR) na Shirika na Maendeleo la Marekani (USAID) kupitia  Mradi wa USAID Afya Yangu Kanda ya Kusini, inasaidia Vituo 135 Sawa na asilimia 89.4 kati ya 151 vinavyotoa Huduma za Kliniki ya Tiba na Matunzo (CTC) Katika Mkoa.

Amebainisha kuwa kati ya fedha zitakazotolewa   kiasi cha TZS.3,072,313,570.85 Sawa na asilimia 74.2 zitatolewa kwa Taasisi za Serikali  ukiwemo Mkoa na Halmashauri zake zote.

Hata hivyo amesema kiasi cha  shilingi 259,915.70 sawa na asilimia 6.2 zitatolewa kwa vituo viwili vya Mashirika ya Dini (FBO), na  shilingi 810,311,504.00 sawa na asilimia 19.6 zitatolewa kwa Asasi ya Kiraia ya ROA inayofanya kazi Katika Halmashauri zote.

Naye Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma  Hilda  Ndambalilo, amesema Mradi wa USID Afya Yangu Kanda ya Kusini unalenga kusaidia na Serikali ya Tanzania Kutoa Huduma bora jumuishi za matunzo , matibabu, na kuzuia maambukizi ya VVU na Kifua Kikuu ambazo zitaboresha matokeo chanya ya afya, hasa kwa vijana na watoto

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.