• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MILIONI 200 kukamilisha ujenzi kituo cha afya Homera Tunduru

Imewekwa kuanzia tarehe: November 7th, 2023

Mkuu wa wilaya ya Tunduru, Mheshimiwa, Wakili Julius S. Mtatiro amekagua maendeleo ya ujenzi na ukarabati wa kituo cha Afya Juma Homera, kilichopo kata ya Nakayaya wilayani humo.

Kituo hicho cha afya kilianza kujengwa chini ya usimamizi wa aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Mheshimiwa Juma Homera, ambaye kwa sasa ni mkuu wa mkoa wa Mbeya. Mh. Homera alikutana na wadau mbalimbali ambao walichangia na kuunda kamati za usimamizi ili kuanzisha ujenzi wa kituo hicho.

Ujenzi na ukarabati wa mradi huo unagharimu zaidi ya shilingi milioni 200, fedha ambazo zimetokana na mapato ya ndani ya Halmashauri ya wilaya ya Tunduru, ambao unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Januari mwaka 2024.

Mh. Wakili Mtatiro aagiza kampuni ya usambazaji wa umeme (TANESCO) kuhakikisha wanarejesha Transfoma waliyoiondoa maeneo ambayo mradi huo wa ujenzi na ukarabati unaendelea.

“Ninafahamu kwamba TANESCO Tunduru walikumbana na changamoto mbalimbali ndio maana wakaondoa Transfoma iliyokuwa maeneo haya ambayo Mradi wa kituo chetu cha afya unaendelea” Alisema Mh. Mtatiro, “Namwagiza Meneja wa TANESCO Tunduru atafute mbadala wa Transfoma hiyo ili kusaidia mradi huu kukamilika kwa muda uliopangwa”

Kwa upande wake Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Daktari Renatus Mathias, ameishukuru serikali ya awamu ya sita kwa kuendelea kuiwezesha Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru, vilevile amemshukuru Mbunge wa Tunduru Kaskazini Mh. Hassan Zidadu Kungu pamoja na waheshimiwa madiwani wote.

Ujenzi na ukarabati wa kituo cha afya Juma Homera upo katika hatua ya umaliziaji, ujenzi wa kituo hicho ni moja kati ya mikakati ya serikali ya awamu ya sita chini ya Raisi wake Mheshimiwa, Daktari, Samia Suluhu Hassan, katika kuhakikisha wananchi wote wanapata huduma za afya zilizo bora.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.