• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MILIONI 495 kufungua barabara mpya Namtumbo

Imewekwa kuanzia tarehe: August 25th, 2022


WAKALA wa barabara za vijijini na mijini(Tarura) wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma,umeishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kuipatia jumla ya Sh.milioni  495,000,000 kwa mwaka wa fedha 2020/2021 zilizotumika kujenga na kuboresha  miundombinu ya barabara wilayani humo.

Pongezi hizo zimetolewa jana na Meneja wa Tarura wilaya ya Namtumbo Mhandisi Fabian Lugalaba, wakati akizungumza kuhusiana na barabara mpya  zilizojengwa na Tarura ambazo zimewezesha kuunganisha vijiji  mbalimbali na kuchochea uchumi wa wananchi.

Lugalaba alisema, kati ya fedha hizo Sh.milioni 90,000,000 zimetumika kwa ajili ya kujenga(kutoboa) barabara mpya na kiasi cha Sh.milioni 405,000,000  zimetumika kujenga madaraja yaliyowezesha kurudisha mawasiliano kwa vijiji vya Mgombasi,Miembeni na Likuyumandela.

Kwa mujibu wake,katikati ya kata ya Mgombasi na Likuyuseka kuna kijiji cha Miembeni ambacho hakikuwa na mawasiliano ya barabara,hivyo kusababisha wakazi wake kuwa na mazingira magumu pindi wanapohitaji kwenda maeneo mengine kwa ajili ya kupata huduma ikiwamo ya afya.

Alisema,kutokana na changamoto hiyo serikali  iliona umuhimu wa kupeleka barabara  katika maeneo hayo ambapo katika bajeti ya mwaka wa fedha 2020/2021 ilitenga jumla ya Sh.milioni 90 kwa ajili ya kutoboa(kujenga)barabara mpya itakayounganisha kata hizo na kijiji hicho.

Lugalala alitaja barabara hizo ni Mfuate-Miembeni-Mgombasi  yenye urefu wa km 17.2 iliyogharimu juma ya Sh.milioni 50 na barabara ya Likuyumandela-Miembeni  yenye urefu  km 11.5 iliyojengwa kwa gharama ya Sh.milioni 40.

Aidha alisema,katika maeneo hayo yote mawili kuna mito ambayo  ilihitaji kujengwa madaraja,ambapo katika barabara ya Mfuate-Miembeni- Mgombasi kulihitaji daraja la mita 20 katika mto Luegu na limejengwa kwa gharama ya Sh.milioni 350.

Lugalaba  alitaja daraja  lingine ni la mita 8 linalounganisha kijiji cha  Miembeni kwenda Likuyumandela ambalo hadi kukamilika limegharimu sh.milioni 40.
Alieleza kuwa,kwa kutumia fedha zinazoletwa na Serikali zikiwamo za ongezeko la tozo zilizoasisiwa na Rais Samia Suluhu Hassan, watahakikisha wanajenga miradi ya barabara kwa ubora wa hali ya juu,uaminifu,uadilifu na inayoendana na thamani halisi ya fedha zinazotolewa ili wananchi wengi hasa waishio maeneo ya vijijini wafikiwe na mtandao wa barabara.

Alisema,malengo ya Tarura ni kuhakikisha maeneo yote ambayo hayafikiki kwa urahisi wanatumia fedha zinazotengwa na Serikali kufikisha huduma ya mawasiliano ya barabara ili kuwarahisishia wananchi kufanya shughuli zao za maendeleo.
Amewaomba wananchi ambao  barabara na madaraja yamejengwa,kuhakikisha wanatunza miundombinu hiyo na kila mmoja kuwa mlinzi kwa mwenzake ili iweze kudumu na kwa muda mrefu.
Baadhi ya wananchi wa kijiji cha Likuyumandela,Mfuate na Miembeni, wameishukuru serikali kwa jitihada za kurudisha mawasiliano  ya barabara katika maeneo hayo.
Ali Mtima mkazi wa kijiji cha Miembeni alisema,kabla ya kujengwa kwa daraja katika mto Luegu linalounganisha kijiji hicho na Mgombasi,walilazimika kupita kwa shida katika mto huo wenye maji mengi hasa kipindi cha masika.


Mtima alisema,baadhi ya watu wamepoteza maisha kwa kusombwa na maji pindi wanapohitaji kwenda kijiji jirani cha Mgombasi kufuata huduma mbalimbali za kijamii ikiwamo huduma za afya.
Issa Amir mkazi wa Mgombasi, ameishukuru Tarura kwa kujenga barabara zinazounganisha kata ya Mgombasi na Likuyu kwani zimerahisisha mawasiliano na kuchochea  kukua kwa uchumi wa wananchi wa maeneo hayo.

Alisema baada ya kujengwa kwa barabara hizo, sasa wanasafirisha mazao kutoka mashambani kwenda sokoni kwa urahisi na wafanyabiashara wengi wanafika kwa ajili ya kununua mazao  wanayozalisha.
MWISHO.



6 Attachments  •  Scanned by Gmail




Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.