• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MSITU wa Taifa wa Mwambesi hazina ya asili inayong,aa mpakani mwa Tanzania na Msumbiji

Imewekwa kuanzia tarehe: April 26th, 2025

Na Albano Midelo

Ukiwa pembezoni mwa Mto Ruvuma, ambao pia ni mpaka wa asili kati ya Tanzania na Msumbiji, unasimama kwa fahari Msitu wa Hifadhi ya Taifa wa Mazingira Asilia Mwambesi  ni hazina iliyofichwa ya viumbe hai, historia, na vivutio vya kipekee vya asili.

Msitu huu mkubwa wenye zaidi ya hekta 112,000 uliopo wilayani Tunduru mkoani Ruvuma, ulianzishwa mwaka 1956, na kupandishwa hadhi kuwa msitu wa taifa katika mwaka 2017/2018. Kupandishwa hadhi huku kunalenga kulinda bioanuwai tajiri inayopatikana hapa, inayojumuisha mamia ya spishi za wanyama, ndege, na mimea adimu duniani.

Viumbe Adimu na wa Kipekee

Meneja wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Wilaya ya Tunduru, Denis Mwangama, anasema Mwambesi si tu kimbilio la wanyamapori kama simba, tembo, swala, nyati, nyani na chui, bali pia ni makazi ya ndege wa kipekee duniani anayeitwa Pentiole.

 Utafiti wa mwaka 2015 uliofanywa na PALMS Foundation umebaini kuwa ndege huyu mdogo mzuri alihamia kutoka Madagaska baada ya makazi yake kuharibiwa na shughuli za binadamu.

Ndege huyu husifika kwa tabia ya kipekee – huogelea kwenye mawimbi ya maporomoko ya maji, akisaka samaki hai ambao ndio mlo wake pekee. Anaonekana zaidi kwenye Maporomoko ya Sunda, yaliyoko ndani ya hifadhi, sehemu ambayo pia ni kivutio kikubwa cha watalii.

“Tanzania tuna bahati kuwa na ndege wa pekee duniani, Pentiole, ambaye anaishi ukingoni mwa maporomoko ya Sunda Waterfalls,” anasisitiza Mwangama.

Historia Iliyofichwa Ndani ya Mapango

Maporomoko ya Sunda si kivutio cha sasa pekee, bali pia ni eneo lenye historia nzito ya vita ya Majimaji (1905–1907).

Mwangama anasema mapango yaliyo juu ya maporomoko hayo yalitumika na wapiganaji kujificha wakati wa vita, na Mto Ruvuma ulikuwa tegemeo kubwa la maji kwa wapiganaji chini ya uongozi wa Kinjeketile Ngwale.

Aidha, kuna ushahidi kuwa Mto Ruvuma ulikuwa njia kuu ya biashara ya meno ya tembo na watumwa iliyotumiwa na Wajerumani na Waarabu waliovuka kutoka Msumbiji. Eneo hili linaonekana kuwa makutano ya historia, urithi wa asili, na maisha ya kisasa ya uhifadhi.

Mazingira Yanayovutia Utalii wa Kiikolojia

Deborah Mwakanosya, mwakilishi wa Meneja wa Msitu huo, anasema Mwambesi ni msitu wa pili kwa ukubwa nchini baada ya Kilombero. Ukiwa umezungukwa na Mto Ruvuma, msitu huu unasheheni mimea adimu kama mipozipozi, miti yenye tabia ya kipekee ya kudondosha maji kutoka kwenye matawi yake, aina ambayo inapatikana katika maeneo machache duniani.

Msitu huu pia ni makazi ya wanyama wa mtoni kama mamba na viboko, ambao huonekana kwa wingi hasa wakati wa masika, wakivutia wageni wanaofika kutalii.

Watalii wanaopenda matukio wanaweza kufurahia utalii wa kuteleza kwa mitumbwi kwenye Mto Ruvuma, huku wakishuhudia mandhari murua ya fukwe za asili zilizo kando ya mto.

Kutoka Kambi ya Uwindaji hadi Kituo cha Uhifadhi

Kabla ya kutangazwa kuwa hifadhi, Mwambesi ulikuwa na vitalu vya uwindaji wa kitalii vilivyokuwa chini ya Kampuni ya Tandara Hunting Safaris, iliyokuwa na kambi maarufu ya wawindaji iitwayo Big Game. Lakini sasa, matarajio mapya yamechipua – uhifadhi wa mazingira na ukuzaji wa utalii endelevu.

“Msitu huu ni hazina ya taifa. Tuna kila sababu ya kuutangaza na kuulinda, kwa ajili ya sasa na vizazi vijavyo,” anahitimisha Mwangama.

Msitu wa Mwambesi si tu mapafu ya Kusini mwa Tanzania bali ni urithi hai unaoelezea hadithi ya asili, mapambano, na matumaini mapya.

 Katika ulimwengu unaopoteza kasi ya uhusiano wa binadamu na mazingira, Mwambesi unasimama kama kielelezo cha matumaini na mfano bora wa uhifadhi unaozingatia historia, tamaduni, na maisha ya sasa.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • BODI ya kwanza ya maji yazinduliwa Tunduru

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.