• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MITI ya asili 3500 yapandwa kwenye uzinduzi wa wiki maalum ya upandaji miti Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: January 3rd, 2023

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas amezindua wiki maalum ya upandaji miti katika Mkoa wa Ruvuma ambapo jumla ya miti ya  asili 3500 imepandwa.

Uzinduzi wa zoezi hilo umefanyika  katika vyanzo viwili ambavyo ni chanzo cha Mto Luegu kilichopo katika Kijiji cha Ngwinde Kata ya Litola Wilaya ya Namtumbo na chanzo cha Mto Mgugusi kilichopo hifadhi ya Lugumbilo Kata ya Mbingamhalule Wilaya ya Songea.

Katika chanzo cha mto Luegu jumla ya miche ya miti ya asili 1500 imepandwa na katika chanzo cha Mto Mgugusi jumla ya miti ya asili 2000 imepandwa kwenye chanzo hicho. Miche ya miti hiyo imetolewa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS).

Mkuu wa  Wilaya ya Namtumbo Dkt.Julius Ningu amesema  wilaya hiyo inatekeleza  maagizo ya kuhifadhi vyanzo vya maji kama yalivyotolewa na Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan ambapo kwa kuanzia amesema wameamua kupanda miti kwenye  chanzo cha Mto Luegu na kuendelea kwenye mito yote inayoingiza maji kwenye mto huo.

Akizungumza baada ya kuzindua upandaji miti kwenye chanzo cha Mto Luegu,Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas amekitaja chanzo hicho kuwa kina umuhimu mkubwa kitaifa kwa sababu Mto Luegu unachangia maji asilimia 19 katika Mto Rufiji.

“Mto huu Luegu ambao tumekuja leo kupanda miti kwenye chanzo chake unachangia asilimia 19 ya maji yote yanayokwenda kwenye bwawa la Mwalimu Nyerere kupitia Mto Rufiji,tunatarajia mradi huu ukikamilika unakwenda kumaliza tatizo la upungufu wa nishati ya umeme nchini’’,alisisitiza RC Thomas.

Amesema kutokana na umuhimu wa chanzo hicho  amepiga marufuku shughuli zote za kibinadamu kwenye chanzo cha Mto huo ili kiwe endelevu.

Hata hivyo amewapongeza wananchi wa Kijiji cha Ngwinde kwa kulinda hifadhi ya msitu huo wenye chanzo hicho ambapo ametoa rai kwa TFS kuwagawia bure wananchi hao miche ya asili nay a matunda ili waweze kupanda na kuhifadhi mazingira.

Akizungumza baada ya kuzindua upandaji miti chanzo cha Mto Mgugusi unaomwaga maji yake katika Mto Ruvuma,Mkuu wa Mkoa amesikitishwa na uharibufu mkubwa wa hifadhi ya msitu wa Lugumbilo uliopo kwenye chanzo hicho ambapo wananchi wamelima na kuharibu chanzo hicho.

Amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Songea  kuhakikisha watu wote waliohusika na uharibifu wa chanzo hicho wakamatwe na kufunguliwa mashtaka kwa sheria ya kuharibu hifadhi ya mazingira na kwamba wote waliolima mashamba ya mahindi kwenye chanzo hicho waondolewe na hifadhi ibaki wazi.

Ameagiza milima yote ya hifadhi katika Mkoa wa Ruvuma ambayo imevamia na wananchi wakifanya shughuli za kibidamu wote waondolewe ili kulinda vyanzo vya maji kwa faida ya kizazi cha sasa na kijacho.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Ruvuma Komred Odo Mwisho akizungumza baada ya kupanda miti kwenye vyanzo hivyo amekemea uharibufu wa mazingira kwenye chanzo cha Mbingamhalule na ameunga mkono hatua za serikali  kuwachukulia hatua wote wanaoharibu mazingira.

Naye Mshauri wa Maliasili Mkoa wa Ruvuma Africanus Challe amesema katika wiki maalum ya upandaji miti inayoanzia Januari Mosi hadi 7,2023 katika Mkoa wa Ruvuma inatarajiwa kupandwa miche ya miti ya asili 1,100,000  iliyotolewa na TFS .

Imeandikwa na Albano Midelo wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.