• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MJI wa Peramiho kupimwa viwanja 5260

Imewekwa kuanzia tarehe: September 14th, 2020

Halmashauri ya Wilaya ya Songea kupitia Idara ya Mipango mji kwa kushirikiana na  Shirika lisilo la kiserikali la Aga Teo Hope Foundation wanatekeleza mradi wa urasimishaji wa viwanja 5260 katika mji mzima wa Peramiho.

Afisa Mipango Miji wa Halmashauri hiyo Meliladius Aliefao  anasema zoezi hilo limelenga kurasimisha mji mzima wa Peramiho ambapo anasema Taasisi ya Aga Teo Hope Foundation imeletwa kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI kuhakikisha kila kipande cha ardhi katika mji wa Peramiho na Halmashauri ya Wilaya hiyo vinapimwa.

“Mkoa wa Ruvuma umewekewa lengo la kurasimisha kwa mwaka watu 7000,sisi kama Halmashauri tumejiwekea ndani ya miezi mitatu kutoka sasa  kurasimisha viwanja wananchi zaidi ya 5000’’,anasema Aliefao.

Anasema hadi kufikia Desemba mwaka huu  watu zaidi ya 5000 watakuwa  wamerasimishwa viwanja vyao kwa kupimiwa, kupangiwa na kumilikishwa na kwamba katika zoezi hilo wananchi wanachangia gharama kulingana na mkubaliano baina ya Halmashauri,Taasisi ya AgaTeo na wananchi wenyewe.

Afisa Mipango Miji huyo anasema wananchi wamekubali kuchangia kiasi cha shilingi 150,000 ambayo hawatalazimika kuichangia kwa mara moja kwa sababu Taasisi ya Aga Teo imefadhili sehemu kubwa ya gharama zinazohitajika kutekeleza mradi huo.

Anasema hadi sasa tayari wananchi wameunda Kamati zao na kufungua akaunti zao ambazo wataweka michango yao taratibu na kwamba wananchi watalazimika kukamilisha michango yao hadi hapo Halmashauri itakapokamilisha hati zao.

Kwa  upande wake William Mapunda ambaye ni Mratibu wa Taasisi ya Aga Teo Hope Foundation anasema wanatekeleza mradi wa urasimishaji wa viwanja katika Halmashauri ya Songea na kwamba Taasisi hiyo ilisajiriwa kwa mujibu wa sheria mwaka 2019 kupitia TAMISEMI na kazi kubwa ya Taasisi hiyo ni kurasimisha ardhi na mashamba katika miji na vijiji.

Mapunda anasisitiza kuwa wamedhamiria kuhakikisha kuwa wananchi wanapata hatimilki ambazo zitawezesha kukopesheka na Taasisi za kifedha kwa upande wa pembejeo za kilimo ikiwemo mbolea na mbegu.

Anazitaja kata sita ambazo wanaanza kutekeleza mradi wa urasimishaji ardhi kuwa ni Kata ya Peramiho,Liganga, Kilagano, Litisha,Parangu na Mbingamhalule.

Imeandikwa na  Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Septemba 14,2020

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBINGA-MBAMBABAY : barabara inayojenga utalii kwenye milima ya Kusini

    June 01, 2025
  • PICHA ya Rais Samia yapamba mti wa kihistoria Namtumbo

    June 01, 2025
  • TAIFA lamlilia Songambele Shujaa wa Uhuru aliyeishi karne moja

    June 01, 2025
  • SHAMBA la AVIV Tanzania ni mfano wa kuigwa nchini

    June 01, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.