Mkoa wa Ruvuma umeendelea kuthibitisha nafasi yake kama ghala kuu la chakula nchini Tanzania, kutokana na uzalishaji mkubwa wa mazao ya chakula unaotokana na ardhi yenye rutuba na juhudi za wakulima. Mazao kama mahindi, mpunga, maharage, viazi na mihogo huzalishwa kwa wingi, na mengi huuzwa nje ya mkoa na hata nchi jirani, hivyo kuufanya Ruvuma kuwa miongoni mwa mikoa michache inayoongoza kwa usalama wa chakula na tija ya kilimo.
Ufanisi huu umetokana pia na jitihada za serikali ya mkoa kwa kushirikiana na Halmashauri zote katika kuweka mazingira wezeshi kwa wakulima, ikiwemo upatikanaji wa pembejeo kwa wakati, elimu ya kilimo bora kupitia maafisa ugani, na ujenzi wa miundombinu kama barabara za vijijini na masoko ya mazao. Uwekezaji huu umeongeza uzalishaji na kupunguza upotevu wa mazao baada ya mavuno.
Zaidi ya kuwa kitovu cha uzalishaji wa chakula, Ruvuma imeanza pia kuvutia wawekezaji katika viwanda vya kuchakata mazao ya kilimo kama vile kiwanda cha kuchakata mahindi na mpunga, jambo linaloongeza thamani ya mazao ya wakulima. Kwa mwenendo huu, Ruvuma si tu kwamba ni gwiji la chakula leo, bali inaendelea kujijengea msingi thabiti wa kuwa kitovu cha usalama wa chakula kwa taifa kwa miaka mingi ijayo.
Regional Commissioner Office
Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.
Simu: 0252602256
Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174
Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz
Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.