• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKOA wa Ruvuma ulivyoingia kumi bora mashindano ya mbio za Mwenge wa Uhuru 2023

Imewekwa kuanzia tarehe: April 9th, 2024

Mkoa wa Ruvuma umeshika nafasi ya kumi kitaifa kati ya mikoa 26  nchini kwenye mashindano ya mbio za Mwenge wa Uhuru 2023.

Hayo yamesemwa na Mratibu wa Mwenge wa Uhuru Mkoa wa Ruvuma Zuberi Mshamu wakati anatoa taarifa ya tathimini ya mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2023 kwenye maandalizi ya Mbio za mwenge wa Uhuru 2024 katika ukumbi wa Manispaa ya Songea ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas Ahmed.

Mshamu amebainisha kuwa katika mashindano ya Mwenge wa Uhuru kitaifa 2023 Mkoa wa Ruvuma ulipata alama 76.27 na kushika nafasi ya kumi  ambapo kimkoa Halmashauri ya Mbinga mji iliyoongoza kwa alama 82.98 na kwamba Halmashauri hiyo imeshika nafasi ya 14 kitaifa.

Kulingana na Mratibu huyo Halmashauri ya Manispaa ya Songea kimkoa imeshika nafasi ya pili kwa alama 80.06 ambapo kitaifa imeshika nafasi ya 37,Halmashauri ya Tunduru ya tatu ikiwa na alama 77.96,kitaifa ikiwa imeshika nafasi ya 53 na Halmashauri ya Namtumbo imeshika nafasi ya nne kimkoa ikiwa na alama 77.82 na kitaifa ikiwa imeshika nafasi ya 55.

Kwa mujibu wa Mratibu huyo,Halmashauri ya Madaba kimkoa imeshika nafasi ya tano ikiwa na alama 74.93,kitaifa imeshika nafasi ya 107,Halmashauri ya Mbinga kimkoa imeshika nafasi ya sita ikiwa na alama 73.57 ambapo kitaifa imeshika nafasi ya 130,Halmashauri  ya Songea kimkoa imeshika nafasi ya saba ikiwa na alama71.86 ambapo kitaifa imeshika nafasi ya 152 na Halmashauri ya Nyasa kimkoa ya nane ikiwa na alama 71  na kitaifa ya 159.

“Timu ya uratibu ya Mkoa inatoa pongezi kwa uongozi wa Wilaya zote na wananchi kwa ujumla kwa kazi kubwa ya kufanikisha mbio  za Mwenge wa Uhuru kitaifa 2023  na mwaka huu tuongeze bidii Zaidi kuhakikisha mwaka 2024 tufanya vizuri zaidi’’,alisisitiza Mshamu.

Mwenyekiti wa Kikao hicho ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas Ahmed akizungumza  kwenye kikao cha maandalizi ya mapokezi ya Mwenge wa Uhuru 2024 mkoani Ruvuma ameagiza kuhakikisha miradi itakayochaguliwa kupitiwa na Mwenge wa Uhuru inakuwa na ubora na kukidhi vigezo vyote.

Amesisitiza mambo ya msingi na vigezo vyote vilivyowekwa na Mwenge wa Uhuru mwaka huu kuzingatiwa na kufanyiwa kazi ikiwemo uhifadhi wa mazingira na uendelevu wa upandaji miti katika wilaya zote mkoani Ruvuma.

“Mwenge ni nembo ya ishara inayomwakilishi Mheshimiwa Rais kwa hiyo inatakiwa kujitoa kikamilifu jambo ambalo ni heshima yetu ya utii kwake hata kama hayupo chombo kile kinamwakilisha yeye’’,alisistiza Kanali Abbas.

Mwenge wa Uhuru unatarajia kuanza mbio zake mkoani Ruvuma Juni 8,2024 na kukamilisha mbio zake Juni 16,2024 ambao utakimbizwa katika Wilaya tano na Halmashauri nane.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.