• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKOA wa Ruvuma umefunguka,wananchi wa Msumbiji na Malawi wanapanda ndege Songea

Imewekwa kuanzia tarehe: October 1st, 2023

WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa amesema baada ya serikali kuboresha uwanja wa ndege wa Songea baadhi ya wananchi wa Malawi na Msumbiji wanatumia kiwanja  hicho kupanda ndege Kwenda Dar es salaam.

Mheshimiwa Majaliwa ameeleza hayo wakati anazungumza kwenye kilele cha Jubilei ya miaka 125 ya uinjlishaji wa kanisa katoliki Jimbo Kuu la Songea iliyofanyika Abasia ya Peramiho nje kidogo ya mji wa Songea ambapo Waziri Mkuu alikuwa ni mgeni rasmi.

“ Baba Askofu Mkoa wa Ruvuma hivi sasa una fursa nyingi ambazo kanisa pia mnaweza kuzitumia,serikali imeboresha na kuimarisha uwanja wa ndege wa Songea,taa za kuwezesha ndege kutua mchana na usiku zimewekwa  na baada ya kuanzisha safari za ndege mara tatu kwa wiki tumegundua kuwa watu wa Msumbiji na Malawi wanafika hapa kupanda ndege na Kwenda Dar es salaam’’,alisisitiza Waziri Mkuu.

Amesema mji wa Songea hivi sasa umetengeneza mzunguko hadi nchi jirani hivyo serikali inalazimika kuongeza safari za ndege kutoka mara tatu hadi  walau mara tano kwa wiki hivyo ametoa rai kwa Mkurugenzi wa ATCL kuona uwezekano wa  kuongeza ndege kwa kuwa zilizopo zinajaa na hazitoshi kwa mahitaji ya wananchi.

Akizungumza kwenye Jubilei hiyo Waziri Mkuu amezitaja fursa nyingine za kiuchumi zilizopo katika Mkoa wa Ruvuma ambazo madhehebu ya dini yanaweza kuzitumia kuwa ni  sekta ya kilimo ambapo amesema Mkoa wa Ruvuma ni miongoni mwa mikoa mitano bora inayoongoza kwa kuzalisha mazao chakula nchini.

Amesema serikali inaendelea na mikakati yake ya kufungua fursa za kibiashara kwenye Mkoa wa Ruvuma ambapo tayari umeme wa gridi umeunganishwa mkoani Ruvuma na kwamba Mkoa umeunganishwa kwa barabara za lami katika wilaya zote na sasa kazi ya kuunganisha barabara za lami ndani ya wilaya inaendelea.

Fursa nyingine amezitaja kuwa ni fursa ya madini,misitu,utalii na uvuvi ambapo ametoa rai kwa madhehebu ya dini kuangalia fursa zilizopo katika maeneo hayo na kwamba serikali ipo tayari kutoa leseni ili madhebeu ya dini yaanze mara moja kutumia fursa hizo.

Waziri Mkuu amesisitiza kuwa serikali ipo tayari kushirikiana na viongozi wa dini ambapo  amempongeza Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Songea Mhashamu Damian Dallu kwa kuadhimisha jubilei ya miaka 125.

 Amesema katika kipindi chote hicho kanisa limefanikiwa kuwajenga waumini wake kiimani na kuwaelimisha  namna waumini wanavyoweza kukuza uchumi wa mtu binafsi.

Ameongeza kuwa katika kipindi hicho kanisa limekuwa mstari wa mbele kuunga mkono kwa vitendo jitihada za serikali za kuwaletea wananchi maendeleo kwa kujenga shule,vituo vya afya,viwanda,vituo vya kulelea Watoto yatima,kuanzisha vyuo mbalimbali vya ufundi stadi  na kuanzisha vyuo vikuu ambapo amesisitiza kuwa kazi hiyo imeleta maendeleo makubwa katika ustawi wa jamii.

Awali akizungumza kabla ya Waziri Mkuu kuzungumza Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Songea Mhashamu Damian Dallu  amesema kanisa  linaadhimisha jubilei ya uinjilishaji iliyoletwa na wamisionari wabenediktini mwaka 1898  likiwa limepata mafanikio makubwa kimwili na kiroho kutokana na  wamisionari wabenediktini kupanda mbegu ya  injili  iliyozaa matunda kwa kipindi cha miaka 125.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas akizungumza kwenye jubilei hiyo amesema Serikali kwa kushirikiana na kanisa  wameweza kuleta mafanikio makubwa kwa wananchi katika sekta za elimu,afya,barabara na miundombinu na kwamba serikali ya Mkoa ipo tayari kuendelea kushirikiana na viongozi wa dini ili kuendelea kuleta maendeleo kwa wananchi.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Peramiho   Mheshimiwa Jenista Mhagama  amesema Jubilei hiyo imeweka historia nyingine kwa kutimiza miaka 125 ya uinjilishaji ambao ulianzia Peramiho mwaka 1898.

Amebainisha kuwa jubilei ya miaka 125 inakwenda kufungua aina mpya ya utalii wa hija hivyo mji wa Peramiho unatarajia kuanza kupokea wageni wengi wa kitaifa na kimataifa ambayo watakuwa wanafika  kufanya utalii wa hija.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.