• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKOA wa Ruvuma waadhimisha Muungano kwa kufanya usafi

Imewekwa kuanzia tarehe: April 27th, 2022

MKOA wa Ruvuma umeadhimisha miaka 58 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kwa kufanya mazoezi  na  usafi wa mazingira  katika  Wilaya zote.

Akizungumza kwenye viwanja vya Soko Kuu la Songea,baada ya kukamilika kwa zoezi la usafi Manispaa ya Songea,Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mhe. Pololet Mgema  aliwataja waasisi wa Muungano kuwa walipigania Uhuru wa nchi yetu na kufanikiwa kuunganisha nchi mbili kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

”Muungano wetu umedumu kwa miaka 58,na umeendelea kuimarika,amani na umoja tulionao leo watanzania ni matunda ya waasisi wa Taifa letu tunawashukuru sana ’’,Alisisitiza Mkuu wa Mkoa.

 Maadhimisho hayo yaliaanza saa 12:30 Asubuhi kwenye ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa kuanza na mazoezi ya kukimbia kuelekea katika maeneo ya kufanya usafi katika masoko mawili ya Manzese na Soko kuu la Halmashauri ya Manispaa ya Songea.

Akizungumzia usafi wa mazingira,Mkuu wa Mkoa amewataka wananchi kuendelea kufuata utamaduni wa kufanya usafi katika maeneo wanayoishi na wanayofanyia biashara na kwamba usafi ni ishara ya tabia njema kuufanya mji wa Songea kupendeza.

“Sisi wanaruvuma tulikwishajiwekea utamaduni wa kufanya usafi siku zote katika maeneo yetu, na maeneo ya umma lakini Ndugu zangu siku za karibuni utamaduni huo umeanza kufifia ndio maana tukasema tutumie siku ya leo kukumbushana wajibu wakufanya usafi”, alisisitiza.

Hata hivyo Mkuu wa Mkoa  amewahimiza wananchi kufanya usafi  kila siku ili kuepuka magonjwa yatokanayo na uchafu  na kwamba gharama za matibabu ziko juu hivyo ni vyema kujijengea tabia ya kufanya usafi  maeneo ya kuishi na maeneo ya kazi ili kupunguza uwezekano wa kupata magonjwa ya kuambukiza.

Pia amesisitiza kufanya  mazoezi ya viungo  kila Jumamosi  ili  kuendelea kulinda afya  na kupunguza magonjwa yasiyoambukiza kila kisukari na shinikizo la damu.

Awali Katibu Tawala wa Mkoa  wa Ruvuma Ndugu Stephen Ndaki akizungumza kwenye maadhimisho hayo alisema kila mwaka Siku ya Muungano imekuwa ikiadhimishwa kwa  kufanya shughuli mbalimbali ambapo mwaka huu katika Mkoa wa Ruvuma siku hiyo imeadhimishwa kwa kufanya usafi wa mazingira na mazoezi.

Amesisitiza wananchi kuendelea kufanya usafi wa mazingira kila siku badala ya kusubiri Siku ya Muungano ambapo amesema katika masoko ya Manispaa ya Songea hali ya usafi hairidhishi hivyo ameagiza wananchi wote kufanya usafi.

Naye Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea Philipo  Beno alisema uzalishaji wa taka katika Manispaa ya Songea umeongezeka  na unakadiriwa kufikia  tani 80 kwa siku wakati uwezo wa Halmashauri kuzoa taka ni tani kati ya 50 hadi 60 kwa siku.

Hata hivyo amesema Manispaa ya Songea imejipanga na kuweka mikakati ya kuhakikisha taka zote zinazolewa kila siku kwa kuongeza magari ya kuzolea taka na kuanzisha kampuni binafsi ya kuzoa taka.

Maadhimisho ya Muungano yametimiza miaka 58 toka kuunganishwa kwa nchi mbili kati ya Tanganyika na Zanzibar chini ya waasisi  Mwl. Julius Nyerere na Sheikh Abeid Amani Karume.

Imeandaliwa na Jackson Mbano 

Kutoka Kitengo cha Mawasilano Serikalini Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Ruvuma

Aprili 27, 2022

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.