• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma aagiza Kampuni ya madini kulipa deni la milioni 274

Imewekwa kuanzia tarehe: September 4th, 2020

MKUU wa  Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme ameiagiza kampuni ya uchimbaji makaa ya mawe ya Market Insight Limited  kuanza kazi mara moja ya uchimbaji katika kata ya Ruanda wilayani Mbinga.

Kampuni hiyo ilisimamisha kazi ya uchimbaji tangu Desemba 2019 kutokana na mgogoro  baina ya wabia wa uchimbaji wa madini hayo hali iliyosababisha Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma kuunda Tume ya uchunguzi wa mgogoro huo iliyofanyakazi kwa siku 14.

Akitoa maagizo hayo kwa wadau wa madini mbele ya waandishi wa habari ofisini kwake mjini Songea Mndeme ameuagiza uongozi wa Kampuni hiyo kuanza uzalishaji wa makaa ya mawe kuanzia Septemba 4,2020 na kuhakikisha wanalipa madeni yote wanayodaiwa na serikali.

“Mnadaiwa mrabaha wa zaidi ya shilingi milioni 274,deni hili lilipwe mara moja kuanzia leo, na deni la kodi ya huduma mnalodaiwa na Halmashauri lilipwe mara moja’’,amesisitiza.

Mndeme pia ameagiza madeni mengine ya kodi ambayo Kampuni hiyo inadaiwa  na Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA yalipwe kuanzia sasa na ameagiza Mhandisi wa Madini  wa Kampuni ya Market Insight Limited Fredrick Mwaipopo ambaye anatuhumiwa kukimbia na shilingi milioni 62 za mishahara ya watumishi wa mgodi atafutwe ili kujibu tuhuma hizo.

Mkuu wa Mkoa ameiagiza kampuni hiyo kuanza kuuza makaa ya mawe kwenye viwanda vya ndani ili kupata nishati ya kutosha na ziada inayobaki isafirishwe kwenda nje ya nchi.

Mndeme pia ameagiza  Kampuni hiyo kutoa ajira kwa Watanzania, kuchimba makaa ya mawe yenye viwango ili soko lipanuke, na kuzingatia afya za watumishi wote wanaofanya kazi katika mgodi huo  na usalama wa mazingira ya mgodi huo.

Mkuu wa Mkoa amewaasa wasimamizi wa mgodi huo kutokuwa na migogoro na kwamba wanapotofautiana wamalizane wao kwa kwao chini ya usimamizi wa Afisa madini  wa Mkoa .

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Cosmas Nshenye ameutaka uongozi wa kampuni hiyo kutekeleza maagizo yote ya serikali yaliyotolewa na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, ikiwemo kupima afya ya watumishi wanaofanya kazi katika mgodi huo,kuwapatia vifaa vya usalama kazini vikiwemo Barakoa na buti.

Naye Kaimu Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Ruvuma Jumanne Mohamed Nkana  ameahidi kutekeleza maagizo yote yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma ambapo ameitaka  Kampuni ya Marketi Isight Limited kutekeleza maagizo hayo na kwamba wakiendelea na migogoro watachukuliwa hatua ikiwemo kunyang’nywa leseni za uchimbaji wa madini.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde na Farida Mussa

Ofisi ya Habari ya Mkoa wa Ruvuma

Septemba 4, 2020.

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.