• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma agawa vitambulisho vya wasajiriamali 9000 vilivyotolewa na Rais mwaka huu

Imewekwa kuanzia tarehe: May 22nd, 2020

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amegawa vitambulisho 9000 vya wajasiriamali wadogo kwa wakuu wa wilaya zote ili waende kuvigawa kwa walengwa.

Mndeme amegawa vitambulisho hivyo katika hafla fupi iliyofanyika  nje ya  viwanja vya  ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma mjini Songea   na kushirikisha wakuu wa Wilaya zote,Makatibu tawala ,Maafisa Tehama,Maafisa Biaashara na Meneja wa mamlaka ya mapato Tanzania Mkoa wa Ruvuma.

Akizungumza kabla ya kugawa vitambulisho hivyo Mdeme amesema Rais Dkt John Magufuli ametoa vitambulisho hivyo ambapo mwaka huu, Mkoa wa Ruvuma umepangiwa jumla ya vitambulisho 58,000 na kwamba katika awamu ya kwanza vimeletwa vitambulisho 9000 na kwamba katika  awamu ya pili Mkoa utaletewa vitambulisho 49,000.

Amesema Vitambulisho vitatolewa kwa wajasiriamali wadogo wenye sifa waliopo katika kila Halmashauri ambapo utaratibu wa ugawaji kwa mwaka huu ni wa  kutumia mfumo wa kompyuta  ili kuwawezesha  kutunza kumbukumbu ya wafanyabiashara na watoa huduma.

“Nawaelekeza maafisa Biashara kuhakikisha fomu ya maombi ya kitambulisho inajazwa na pesa inayokusanywa iwekwe Benki ,kila risiti moja ya malipo ya shilingi 20,000 itatumika kusajiri mfanyabiashara mmoja’’,amesisitiza.

Ameutaja mchanganuo wa  mgao wa vitambulisho hivyo mwaka huu katika awamu ya kwanza kuwa Wilaya ya songea imepewa vitambulisho 3,500,Mbinga vitambulisho  2000,Tunduru vitambulisho  1500,Namtumbo vitambulisho 1000,na Nyasa imepata vitambulisho 1000.

 Awali akizungumza kabla ya kumkaribisha Mkuu wa Mkoa,Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma, Steven Ndaki amelitaja lengo la kuwagawa vitambulisho hivyo ni kuwarahisishia wafanyabiashara wadogo katika biashara ili waondokane na usumbufu hivyo kufanya kazi kwa ufanisi.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Mgema  amesema mwaka jana Wilaya ya Songea Ilipewa Vitambulisho 15,000  ambavyo walifanikiwa kuvigawa vyote kwa wajasiriamali wadogo na kwamba mwaka huu wajasiriamali wadogo wanavisubiri vitambulisho hivyo kwa hamu kubwa.

 Mwaka 2019,Rais Dkt John Magufuli aligawa vitambulisho vya wajasiriamali wadogo 60,000 katika Mkoa wa Ruvuma ambapo hadi kufikia Mei 19, mwaka huu Mkoa ulifanikiwa kugawa vitambulisho 55,607 na kukusanya shilingi 1,112,135,000/=

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Mei 21,2020

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.