• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma aongoza kikao cha tathmini ya mfumo wa masoko kupitia vyama vya ushirika

Imewekwa kuanzia tarehe: March 5th, 2020

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amewaagiza wadau  mbalimbali wa ushirika,kuhakikisha kuwa ushirika unastawi kwa manufaa ya wanachama na taifa kwa ujumla.

Mndeme ametoa agizo hilo wakati  anafungua kikao cha tathmini ya mfumo wa masoko kupitia vyama vya ushirika kilichofanyika kwenye ukumbi wa Songea klabu na kushirikisha wadau  kutoka wilaya na Halmashauri zote za Mkoa wa Ruvuma.

Kwa mujibu wa Mndeme,ushirika unalindwa na sera na sheria ya ushirika na kwamba wanachama wenyewe ndiyo wasimamizi wa shughuli za kila siku za ushirika ambapo ameagiza katika Mkoa mzima pawe na mpango kabambe wa kusimamia,kuimarisha na kuendeleza ushirika.

”Tusiwaruhusu wanaotaka kupindisha sheria ili waue mfumo wa ununuzi wa mazao ya ufuta,mbaazi na soya katika Mkoa wetu,tusiwaruhusu wezi na wabadhirifu kuwa viongozi wa vyama vya ushirika’’,alisisitiza Mkuu wa Mkoa.

Amesema msimu wa masoko ya mazao ya jamii ya mikunde,ufuta,soya na mbaazi kwa mwaka 2019/2020 unatarajia kuanza Mei mwaka huu,hivyo ameagiza vyama vya msingi viandae vitendea kazi na vituo vya makusanyo,visimamie na kuanza makusanyo toka kwa wakulima.

Akitoa taarifa ya mazao ya ufuta,soya na mbaazi ,Meneja Mkuu wa SONAMCU Juma Mwanga amesema  katika  msimu wa mwaka 2019/2020 minada ya ufuta ilikuwa 19 yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 16,minada ya soya 10 yenye thamani ya zaidi ya bilioni mbili na minada ya mbaazi mine yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 471.

Hata hivyo licha ya mafanikio yaliopatikana amezitaja changamoto zilizojitokeza katika kipindi hicho kuwa ni kukosekana kwa vifaa vya kusafishia ufuta,bei elekezi ya chini ukilinganisha na bei ya soko na wanunuzi kuchelewa kutoa mzigo ghalani.

Kwa muda mrefu vyama vya ushirika katika Mkoa wa Ruvuma vimekuwa sehemu muhimu ya maendeleo ya Mkoa na Taifa kwa ujumla  kwa sababu ushirika ni njia muhimu ya maendeleo kwa watu wa vipato vyote.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Machi 4,2020

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.