• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKUU wa Wilaya ya Mbinga azindua miongozo ya Elimu

Imewekwa kuanzia tarehe: October 3rd, 2022

MKUU wa wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma Mheshimiwa  Aziza Mangosongo,amezindua miongozo ya usimamizi na uendeshaji wa elimu huku akikemea tabia ya baadhi ya walimu wa kiume kuwa na mahusiano ya kimapenzi na wanafunzi wao.

Mheshimiwa Mangosongo alisema,tabia hiyo imechangia kuporomoka kwa maadili kwani baadhi ya walimu wanatumia nafasi zao kuwarubuni wanafunzi  na kufanya nao mapenzi,hivyo kusababisha wanafunzi kufanya vibaya  katika masomo yao.

MHE.Mangosongo ametoa kauli hiyo,alipokuwa akizungunza na walimu wakuu wa shule za msingi na sekondari na viongozi wa Halmashauri ya wilaya Mbinga kwenye uzinduzi wa miongozo hiyo katika Halmashauri  ya wilaya Mbinga.

“kuna mwalimu mmoja sitaki kutaja jina lake na shule anayofundisha, amempa mimba mwanafunzi wake aliyetakiwa kujiandaa na mitihani ya kidato cha nne mwaka huu,lakini jambo la kusikitisha hata walimu wenzake hawataki kumtaja”alisema Mangosongo.

Alisema,Halmashauri ya wilaya Mbinga hakuna sababu ya kutofanya vizuri katika  suala la kitaaluma kutokana na kuwepo kwa mazingira mazuri ya kujifunzia na kufundishia ikilinganisha na Halmashauri nyingine katika mkoa wa Ruvuma.

Mangosongo alieleza kuwa,miongozo hiyo hususani wa kuimarisha ufundishaji na ujifunzaji ngazi ya elimu ya msingi ni mikakati ya kuimarisha ufundishaji na ujifunzaji,usimamizi na ufuatiliaji na ushiriki wa wadau ili kufanikisha utekelezaji huo.

Hivyo,amewataka walimu wa shule za  msingi na sekondari kutumia miongozo ya usimamizi na uendeshaji  iliyotolewa na serikali kufanya tathimini ya mara kwa mara ya hali ya elimu ili kurudisha heshima ya wilaya ya Mbinga kitaaluma.
Amewaagiza,kuanza kuwafuatilia na kuwaandikisha watoto wote wenye umri wa kuanza elimu ya awali na shule ya msingi ili waanze masomo ifikapo mwezi Januari 2023 na kusimamia watoto watakaochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza wawe wameripoti mara shule zitakapofunguliwa.

Amewahimiza walimu kuwa wabunifu, kujifunza ikiwamo kusoma vitabu mara kwa mara ili kupata maarifa na mbinu mpya zitakazowasaidia kufanya vizuri katika kazi zao za kila siku.

Miongozo iliyozinduliwa katika Halmashauri hiyo,ni mkakati wa kuimarisha ufundishaji na ujifunzaji ngazi ya elimu ya msingi,uteuzi wa viongozi wa elimu katika mamlaka za serikali za mitaa na changamoto katika  uboreshaji wa elimu ya msingi na sekondari.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Juma Haji alisema,wamejipanga  kufanya vizuri katika sekta ya elimu ili watoto wote waliopo  kwenye shule za msingi na sekondari wapate elimu bora na hatimaye waweze kufanya vizuri katika  masomo yao.

Naye Afisa elimu sekondari wa Halmashauri hiyo Peter Ntalamka alisema, Halmashauri ya wilaya Mbinga ina shule za msingi 167 kati ya hizo shule za serikali ni 164, na shule binafsi 3  na kwa upande wa sekondari kuna shule 47 ambapo za serikali 31 na binafsi 16.

Alieleza kuwa, kwa  shule za msingi kuna wanafunzi 67,078 na sekondari 14,652 na mahitaji ya walimu wa shule za msingi 1,936 waliopo 938 pungufu 998 na sekondari mahitaji ya walimu 716 waliopo 535 na pungufu walimu 181.
Aidha alisema, mwaka 2022 uandikishaji kwa wanafunzi wa shule za msingi ulivuka lengo kwa asilimia 133 kwa darasa la awali na asilimia 123 kwa darasa la kwanza.
Kwa mujibu wa Afisa elimu huyo,kwa shule za sekondari uandikishaji ulikuwa asilimia 94 kwa kidato cha kwanza, na asilimia 76 kwa kidato cha tano,hata hivyo juhudi za kuhakikisha wanafunzi wote wanaandikishwa.
MWISHO.



Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.