• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MNDEME aagiza waliosababisha Manispaa ya Songea kupata Hati yenye mashaka wachukuliwe hatua

Imewekwa kuanzia tarehe: May 11th, 2020

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amesikitishwa na kitendo cha Halmashauri ya Manispaa ya Songea kupata hati yenye mashaka na ameagiza wote waliosababisha wachukuliwe hatua.

Mndeme ametoa agizo hilo wakati  anazungumza kwenye kikao maalum cha Baraza la madiwani cha kujadili taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG) kuhusu hoja na mapendekezo ya  CAG kwa Hesabu za Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa mwaka 2018/2019.

Manispaa ya Songea imepata hati yenye mashaka kwa mujibu wa ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa mwaka wa fedha wa 2018/2019 ambapo Mndeme amesema  ripoti hiyo inasikitisha na kuumiza sana.

“Naagiza kuanzia sasa taratibu za kinidhamu zianze kuchukuliwa kwa wale wote waliosababisha Halmashauri  ya Manispaa ya Songea kupata hati yenye mashaka,hatua zichukuliwe bila kujali awe ni Diwani au Mtendaji,suala hili limetutia aibu sana’’,alisisitiza Mndeme.

Mndeme ameagiza ufanyike uchunguzi ili kubainia wote walisababisha kupatikana kwa hati yenye mashaka kwa Halmashauri ya Manispaa ambayo ni kioo katika Mkoa wa Ruvuma na ina kila kitu ukilinganisha na Halmashauri nyingine za Mkoa.

Hata hivyo Mndeme amesisitiza kuwa kupata hati yenye shaka kuwafanye madiwani na watendaji waongeze bidii na kwamba CAG ametoa hoja na mapendekezo ambayo yanafikia idadi ya 54 kati ya hizo Hoja na Mapendekezo yaliyojibiwa na kufungwa ni 11 tu.

Kwa upande wake Mkaguzi Mkuu wa Nje wa Hesabu za Serikali Deogratias Waijaha ameitaja sababu kuu iliyosababisha Halmashauri hiyo kupata Hati yenye mashaka kuwa ni kuripoti shilingi milioni 98 kwenye vitabu vyake vya Hesabu kama mapato ya ndani ambayo majibu yake hayakupatikana.

“Nawashauri kupitia vikao vyenu mfute milioni 98 kama mapato kwa sababu ile fedha itakwenda chanzo kikuu,haitarudi kwenu ,lakini taratibu za kijinai ziendelee kwa wote ambao walitenda hayo makosa  kulingana na sheria za nchi,mlitakiwa kufanya mapema kabla ya kufunga Hesabu’’,alisisitiza Mkaguzi wa Hesabu za Nje.

Waijaha amesisitiza kuwa Manispaa ya Songea ilipata Hati yenye mashaka kwa tukio moja la udanganyifu wa milioni 98 na kwamba Manispaa hiyo haijapata hati chafu kwa sababu vitu vingine vyote vipo sawa.

Hata hivyo amesisitiza kuhakikisha wananunua vifaa kwa watu wenye  risiti za mashine za  EFD ili kuepuka kuendelea  kuandikiwa hoja kutokana na kutumia watu ambao hawana risiti hizo hali ambayo inaikosesha serikali mapato .

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea Alhaj Abdul Hassan Mshaweji kwa niaba ya Madiwani na watendaji ameahidi  kufanyia kazi mara moja maagizo yote ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali.

Licha ya kupata Hati yenye mashaka,Manispaa ya Songea katika kipindi cha mwaka wa fedha wa 2018/2019 imefanikiwa kukusanya mapato ya ndani kwa asilimia 92 na kuweza kuchangia kwa asilimia 100 mfuko wa wanawake,vijana na wenye ulemavu kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 191 mwaka 2018/2019.

Imeandika na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Mei 10,2020

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.