• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MOHAMED Enterprises yasaidia vituo vitatu vya yatima Songea

Imewekwa kuanzia tarehe: February 5th, 2021

KAMPUNI ya Mohamed Enterprise imetoa msaada wa vyakula na sabuni vilivyogharimu zaidi ya shilingi milioni 1.8 kwa vituo vitatu vya kulelea watoto yatima mjini Songea mkoani Ruvuma.

Mwakilishi wa Kampuni hiyo Angel Samasuba akizungumza  mara baada ya kumaliza zoezi la ugawaji wa msaada huo,amevitaja vituo vya kulelea yatima vilivyopata msaada huo kuwa ni Kituo cha SWACCO kilichopo Kata ya Mwengemshindo,St.Anton cha Mfaranyaki na Kituo cha Mchungaji Mwema kilichopo Mjimwema.

Samasuba amesema Kampuni ya Mohamed katika vituo vyote vitatu imetoa jumla ya lita 120 za mafuta ya kula zilizogharimu shilingi  516,000 na mifuko ya unga wa sembe kilo 300 iliyogharimu shilingi 234,000.

Misaada mingine iliyotolewa ni sabuni za miche katoni 12 zenye thamani ya shilingi 120,000,vinywaji aina ya juisi katoni 30 zenye thamani ya shilingi 195,000 na mbuzi sita zenye thamani ya shilingi 600,000.

“Sisi kama Kampuni ya Mohamed Enterprise tumekuwa na kawaida ya kutoa misaada kwa makundi maalum na vituo vya kulelea watoto yatima kwa lengo la kuunga mkono jitihada za serikali za kuwasaidia watu wenye uhitaji ili kuwafariji na kuwatia moyo’’,alisema Samasuba.

Akizungumza mara baada ya kupokea msaada huo Mwakilishi wa kituo cha kulelea yatima  cha Mchungaji mwema cha Mjimwema Sr.Maria Veronika OSB,ameishukuru Kampuni ya Mohamed kwa msaada huo ambao amesema utawasaidia watoto 39 ambao wanalelea na kituo hicho.

Naye Mwakilishi wa kituo cha kulelea watoto yatima cha SWACCO Castrol Whero amesema kitendo kilichofanywa na Mohamed Enterprise kimeleta faraja kubwa kwa sababu yatima ni kundi maalum lililopo katika jamii linalohitaji msaada.

Amesema kituo cha SWACCO kilianza mwaka 2000 kikiwa na watoto 50 ambapo hivi sasa kituo hicho kinalea watoto 23 na watoto 31 wanahudumiwa wakiwa majumbani na walezi wao.

Vinsent Ndumbaro ni Kaimu Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Ruvuma akizungumza kwa niaba  ya serikali,ameipongeza na kuishukuru Kampuni ya Mohamed Enterprise kuunga mkono juhudi za serikali za kuwasaidia watu wenye mahitaji maalum ambapo ametoa rai kwa wadau wengine kuiga mfano huo.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Februari 5,2021

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.