• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MPANGO Jumuishi wahudumu wa afya ngazi ya jamii wabisha hodi Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: December 10th, 2024

Serikali katika kutambua umuhimu wa afya bora kwa wananchi imeendelea kuweka kipaumbele katika huduma za afya zenye ubora na zinazowafikia wananchi popote walipo.

Hayo yamesemwa na Kaimu Katibu wa Mkoa wa Ruvuma Joel Mbewa wakati akisoma hotuba kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Kanali Ahmed Abbas Ahmed, katika mkutano wa utambulisho wa Mpango Jumuishi wa Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii uliojumuisha viongozi wa mkoa, wilaya na halmashauri uliofanyika katika ukumbi wa Hospitali ya Mkoa, Songea (HOMSO) mjini Songea.

"Baada ya Serikali yetu kuwekeza kwa kiasi kikubwa katika miundombinu ya vituo vya kutolea huduma za afya pamoja na vitendea kazi na wataalam, sasa Serikali imekuja na mikakati maalumu ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma na Elimu za afya huko huko walipo," alisema Mbewa.

Ameongeza kuwa Serikali kupitia TAMISEMI inaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kutekeleza mikakati ya kuimarisha huduma za afya nchini ili kufikia huduma ya afya kwa wote ifikapo 2030.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Ofisi ya Rais TAMISEMI na Mlezi wa Mkoa wa Ruvuma katika huduma za afya ngazi ya jamii, Mary Shadrack amesema kazi yao kubwa ni kuwajengea uwezo watoa huduma ngazi ya jamii wa mkoa, halmashauri na waliopo maeneo ya jamii.

Naye Afisa Mpango wa Taifa wa Huduma za Afya Ngazi ya Jamii, Bahati Mwailafu, akiiwakilisha Wizara ya Afya, amesema Mpango huo ulizinduliwa Januari 2024 ukiwa na lengo la kuimarisha huduma za afya ngazi ya jamii na kutatua changamoto mbalimbali zilizokuwa zinajitokeza katika kutoa huduma hizo.

Hata hivyo Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Hilda Ndabalilo amesema anatambua ugumu wa majukumu wa watoa huduma za afya ngazi ya jamii katika maeneo wanayoyaaimamia  ya kutolea huduma hizo.

Ameongeza kuwa licha ya ugumu wa majukumu wanayotekeleza mchango wao hauwezi kubezwa kwani wamekuwa kiungo muhimu kati ya jamii na vituo vya kutolea huduma.

Watoa huduma za Afya ngazi ya jamii ni wananchi wa kawaida ambao wamepewa ujuzi, uhamasishaji na uelimishaji wa jamii lakini hutoa huduma ya kwanza kwa wagonjwa na Rufaa pale zinapohitajika.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.