• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MRADI mkubwa wa maji utakavyoleta neema kwa wakazi wa Nyasa

Imewekwa kuanzia tarehe: October 27th, 2022

MKUU  wa mkoa wa Ruvuma Kanal Laban Thomas,amemuagiza Kaimu Mkuu wa wilaya ya Nyasa Aziza Mangosongo kupitia kama ya ulinzi na usalama,kuwakamata na kuwafikisha mahakamani mafundi wa kampuni ya Emirate Builder Co Ltd waliohusika kuiba vifaa vya ujenzi wa miradi ya maji katika kijiji cha Lituhi na Liuli wilayani humo.

Kanal Laban ametoa agizo hilo kwa nyakati tofauti, wakati alipotembelea ujenzi wa miradi miwili ya maji katika kijiji cha Mwerampya na Liuli wilayani Nyasa inayotekelezwa na Serikali kupitia wakala wa maji safi na  usafi wa mazingira(Ruwasa).

Mkuu wa mkoa,amewataka wananchi kutambua kuwa miradi hiyo ni ya kwao,kwa hiyo wana wajibu wa kuilinda na kuepuka kununua vifaa vinavyoletwa kwa ajili ya ujenzi wa miradi kutoka kwa mafundi.

Alisema,baadhi ya mafundi ndiyo wanaohusika  kuiba vifaa na kuwaomba wananchi kutokuwa sehemu ya watu wanaohujumu miradi hiyo kwani Serikali inatumia fedha nyingi kwa ajili ya kutatua changamoto na kuleta maendeleo.

“hakuna maana  kama Mheshimiwa Rais Samia anaangaika usiku na mchana kutafuta fedha kwa ajili ya kuwaletea maendeleo wananchi,alafu sisi  ndiyo tunakuwa wa kwanza kuiba vifaa vinavyoletwa,tabia hii haikubailiki hata kidogo,nawaomba wananchi  kushirikiana na serikali yenu kuwafichua watu wanaojihusisha na tabia hiyo”alisema Kanal Laban.

Aidha,amemtaka Mkandarasi kampuni ya Emirate Builders Co Ltd, kufanya kazi usiku na mchana ili kukamilisha kazi hiyo kwani wananchi wana hamu kubwa ya kupata  maji safi na salama ili waweze kuyatumia katika shughuli zao za maendeleo.

Kwa upande wake Meneja wa Ruwasa wilaya ya Nyasa  Jeremia Maduhu alisema,Serikali imetoa Sh.bilioni 11,718,087.448 kwa ajili ya kutekeleza miradi miwili ya maji katika kijiji cha Lituhi na Liuli wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma.

Maduhu alieleza kuwa, miradi yote miwili  inajengwa na kampuni ya Emarate Builders Co Ltd na iko katika hatua mbalimbali za utekelezaji wake huku akibainisha kuwa kati ya fedha hizo Sh.bilioni 6,595,019,723 zitatumika kutekeleza mradi wa maji Lituhi  ambapo mkandarasi ameshalipwa shilingi milioni 989,252,958.50.

Kwa mujibu wa Maduhu,mradi  huo utakapokamilika utahudumia vijiji saba vya Lituhi,Kihuru,Nkaya,Mwera mpya, Ndumbi Liweta na Mbaha vyenye takribani wakazi 26,477.

Alisema,katika mradi huo kazi zilizopangwa kufanyika ni ujenzi wa tanki la la kuhifadhia maji la lenye mita za ujazo 500, kujenga vituo 19 vya kuchotea maji, ujenzi wa chanzo,ununuzi wa bomba za urefu wa mita 77.570,kuchimba mitaro na ujenzi wa ofisi ya chombo cha watumia maji.

Alitaja kazi zilizoanza kufanyika ni  ujenzi wa chanzo, ujenzi wa tenki la kuhifadhia maji la lita 500,000 na ununuzi wa mabomba.

Akizungumzi mradi wa maji Liuli alisema,mradi  huo umetengewa jumla ya Sh.bilioni 4,718,087,448 na utahudumia vijiji vitano vya Liuli,Nkalachi,Hongi,Puulu na Mkali A na B na utawanufaisha zaidi ya wakazi 25,808.

Baadhi ya wananchi wameiomba Serikali kuharakisha ujenzi wa mradi huo ili kuwanusuru na adha ya kuamka usiku wa manane kwenda kutafuta maji kwa ajili ya matumizi yao ya kila siku.

Maria Ngailo mkazi wa kijiji cha Mwerampya kata ya Lituhi alisema,tatizo la maji katika kijiji hicho limesababisha hata baadhi ya wanafunzi kukatisha masomo kwa kupata mimba  wanapokwenda kutafuta maji mbali na makazi yao.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.