• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MITI ya mitiki itakavyotengeneza mamilionea wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: December 9th, 2020

Miti ya mitiki itakavyotengeneza mamilionea wilaya ya Nyasa

Programu ya kuendeleza mnyororo wa thamani wa mazao ya misitu (FORVAC) imetoa ruzuku ya miche ya mitiki zaidi ya 81,000 iliyopandwa katika hekta 72.1 kwa wakulima 80  mwambao mwa Ziwa Nyasa mkoani Ruvuma msimu wa mwaka 2019/2020.

Mwenyekiti wa Muungano wa Chama  cha Wazalishaji wa miti ya misaji (mitiki) kijiji cha Liuli wilaya ya Nyasa Samwel Mawanja amesema  FORVAC wanaendelea kufadhili mradi wa miti ya mitiki ambayo inatekelezwa katika vijiji sita mwambao mwa ziwa Nyasa.

“Katika msimu wa mwaka 2020/2021 tumeomba tena FORVAC ruzuku ya miche ya mitiki 300,000 kupitia vijiji sita vinavyozalisha mitiki ambavyo ni Liuli,Nkalachi,Nkali A,Nkali B na Lipingu na Hongi’’,alisema Mawanja.

Amesema mradi wa mitiki ni mradi pekee ambao haujawahi kutekelezwa tangu uhuru mwambao mwa ziwa Nyasa ambao unatarajia kuleta tija kubwa kiuchumi kwa wananchi hivyo kuleta mapinduzi makubwa kiuchumi baada ya miti hiyo kuanza kuuzwa.

Ameyataja matarajio ya wananchi hao ambao pia ni wavuvi katika ziwa Nyasa kuwa ni kutengeneza boti za kisasa kwa kutumia miti ya mitiki zitakazowawezesha kwenda kuvua mbali badala ya kuendelea kuharibu misitu ya asili kwa kukata miti ya kutengenezea mitumbwi.

Kwa upande wake Mratibu wa  FORVAC Taifa Emanuel Msoffe akizungumza baada ya kukutana na kikundi hicho cha wazalishaji mitiki,ametoa rai kwa wananchi mwambao mwa ziwa Nyasa kulinda na kuhifadhi misitu iliyopo kwenye milima ya Livingstone kwa kuacha kulima na kukata miti hovyo.

Amesisitiza kuwa eneo la Mwambao mwa ziwa Nyasa linafaa sana kwa uzalishaji wa mitiki kwa sababu ni eneo ambalo lipo chini ya milima ya livingstone hivyo lina  rutuba nyingi.

“Natoa rai kwa wananchi mwambao mwa ziwa Nyasa kuendelea kupata miti ya mitiki kwa sababu kati ya miaka 15 hadi 20 mtavuna na kupata fedha nyingi zitakazobadilisha kabisa maisha yenu’’,alisisitiza Msoffe.

Ofisa Maliasili wa Halmashauri ya Nyasa Bugingo Bugingo amesema utafiti umebaini kuwa hekari moja ya mitiki inaweza kumuingizia mkulima zaidi ya milioni 400 hivyo ni muhimu wananchi kupanda miti hiyo ili kukuza uchumi wao.

Bugingo anayataja miongoni mwa matumizi ya zao la mitiki  ni kutengenezea vitako vya silaha aina ya bunduki,vyombo vya majini kama vile meli na boti na kutengeneza samani mbalimbali zenye gharama kubwa.

Utafiti umebaini kuwa Mahitaji ya mtiki katika soko la duniani ni makubwa ,ndiyo maana nchi za Ulaya na nchi za Asia zikiongozwa na China na India wananunua miti aina ya mitiki kwa wingi kutoka Tanzania,na hata hatujaweza kufikisha hata robo ya mahitaji yao.

Nchi  ya Malyasia kwa mwaka hupata mapato ya Dola  za Marekani zaidi ya bilioni 13 kutokana na kilimo cha mitiki.Mahitaji ya soko la mitiki ni makubwa hivyo wakulima wapya wa mitiki katika wilaya ya Nyasa na maeneo mengine nchini waongeze uzalishaji wa zao hili,  mahitaji yake yanaendelea kuongezeka.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Desemba 9,2020

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.