• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MSIKIMBILIE hasara,serikali inakuja na bei ya neema kwa mahindi Julai

Imewekwa kuanzia tarehe: May 31st, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma, Mheshimiwa Kapenjama Ndile, amewaonya wakulima wa mahindi katika wilaya hiyo kujiepusha na kuuza mazao yao kwa bei ya hasara kabla ya soko rasmi kufunguliwa mwishoni mwa mwezi Julai. Ametoa wito huo kutokana na hali ya hewa isiyo ya kawaida iliyosababisha mahindi mengi kuharibika, hali inayoweza kudhoofisha ubora na thamani ya zao hilo muhimu kwa chakula na uchumi wa wananchi.

Akizungumza kwa msisitizo mkubwa, Mheshimiwa Ndile amesema mvua zilizoendelea kunyesha hadi wiki ya kwanza ya Mei zimeathiri uhifadhi wa mahindi, na hivyo kuwa na uwezekano mkubwa wa kuwepo kwa mahindi mabovu. “Hata katika kununua, lazima tuwe na uchaguzi makini. Serikali haitapenda kununua mahindi yaliyochafuka, yaliyooza au yenye rangi zisizo za kawaida. Tunahitaji mahindi meupe, safi na bora,” amesisitiza.

Ameshauri sekta binafsi kuwekeza kwenye mashine za kisasa zinazoweza kupepeta na kuchambua mahindi kwa ubora unaohitajika, huku akiwahimiza wananchi kuwa wavumilivu na kutouza kwa haraka mazao yao kwa walanguzi wanaowapunguzia kipato. “Kama kuna shida ya pesa, wauze mazao mengine kama maharage, ufuta au soya. Lakini mahindi wayahifadhi, kwani ndiyo chakula kikuu na serikali italeta bei inayolipa,” amesema Ndile.

Kiongozi huyo ameonesha masikitiko kwa baadhi ya wakulima waliouza mahindi kwa bei ya chini mwaka jana kwa wafanyabiashara kutoka Kenya, kabla ya serikali kutangaza ununuzi rasmi kwa bei ya juu ya shilingi 700 kwa kilo. “Wananchi walikimbilia kuuza kwa Sh350, wengine Sh400. Mwezi mmoja baadaye serikali ikaanza kununua kwa Sh700. Wakaanza kulalamika ‘sikujua, sikujua.’ Hii ni fursa ya kujifunza,” amesema kwa ukali.

Kwa mara nyingine, Mkuu huyo wa Wilaya ameweka bayana kuwa serikali ipo tayari kuwanunulia wakulima mahindi kwa bei ya haki na ya ushindani kuanzia Julai mwaka huu  ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuinua kipato cha wakulima na kupunguza umasikini vijijini. “Tunasimama pamoja nanyi. Lakini ili mnufaike, mnatakiwa kuwa wavumilivu, wasikivu na wapangaji wa muda mrefu,” amehitimisha kwa matumaini.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBINGA-MBAMBABAY : barabara inayojenga utalii kwenye milima ya Kusini

    June 01, 2025
  • PICHA ya Rais Samia yapamba mti wa kihistoria Namtumbo

    June 01, 2025
  • TAIFA lamlilia Songambele Shujaa wa Uhuru aliyeishi karne moja

    June 01, 2025
  • SHAMBA la AVIV Tanzania ni mfano wa kuigwa nchini

    June 01, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.