• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MWENGE wa Uhuru kuanza kukimbizwa mkoani Ruvuma kesho

Imewekwa kuanzia tarehe: April 7th, 2022

MBIO za Mwenge wa Uhuru mwaka 2022 zinatarajia kuanza mbio zake mkoani Ruvuma Aprili 8 mwaka huu.

Akizungumza na wanahabari ofisini kwake mjini Songea,leo ,Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge amesema Mwenge wa Uhuru Aprili 8 unatarajiwa kupokelewa katika kijiji cha Lituhi wilayani Nyasa ukitokea mkoani Njombe.

Brigedia Jenerali Ibuge amesema Mwenge wa Uhuru ukiwa mkoani Ruvuma,utakimbizwa kilometa 1,052.3 ambapo unatarajiwa kutembelea miradi 62 yenye thamani ya Zaidi ya shilingi bilioni tano katika wilaya tano zenye Halmashauri nane.

Amesema Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu zinatarajia kukamilisha mbio zake Halmashauri ya Tunduru Aprili 15 na  Aprili 16,Mwenge huo utakabidhiwa katika kijiji cha Lumesule mkoani Mtwara.

“Kama ilivyo jadi wana Ruvuma,naomba tujitokeze kwa wingi,kwa nderemo na vifijo katika maeneo yote ambayo Mwenge wa Uhuru utapita,pia kujitokeza katika maeneo ya mikesha’’,alisisitiza RC Ibuge.

Hata hivyo Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma amewakumbusha wananchi wote kuendelea kuchukua tahadhari ya ugonjwa wa UVIKO 19 kwa kuvaa na kunawa mikono,sanjari ya kujitokeza katika zoezi la utoaji chanjo ya UVIKO 19 ambalo litaendelea kutolewa katika maeneo yote ya mikesha.

Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2022 zimebeba ujumbe maalum usemao “Sensa ni msingi wa mipango ya maendeleo,shiriki kuhesabiwa,tuyafikie maendeleo ya Taifa’’.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma

Aprili 7,2022

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.