• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

NAIBU WAZIRI ataka Mkandarasi jengo la abiria kiwanja cha Ndege Songea asimamishwe

Imewekwa kuanzia tarehe: February 25th, 2024

Naibu Waziri wa Uchukuzi David Kihenzile ameitaka Mamlaka wa Viwanja  vya Ndege Tanzania (TAA) kuvunja mkataba na Mkandarasi Kampuni ya Manyanya Enginnering Company Limited kutokana na Mkandarasi huyo kushindwa kukamilisha mradi wa jengo la abiria kwa wakati.

Naibu Waziri Kihenzile ametoa maagizo hayo Mkoani Ruvuma mara baada ya kukagua mradi huo na kutoridhishwa na maendeleo ya utakelezaji wake ambao ulitakiwa kuwa umekamilika mwishoni mwa mwaka 2023.

“Serikali imewekeza takribani bilioni 37 ili kuboresha miundombinu mbalimbali katika kiwanja hiki, na mkandarasi wa Jengo la abiria amelipwa muda mrefu fedha za kuanza mradi huu lakini amefanya kazi chache na kutelekeza mradi, hatuwezi kukubaliana na jambo hili ninawaelekeza TAA kuhakikisha mnapitia vipengele vyote vya mradi huu na mvunje mkataba huu maana ameshindwa kukamilisha kwa wakati’ amesema Naibu Waziri Kihenzile.

Naibu Waziri Kihenzile imeitaka TAA kuhakikisha Viwanja vya ndege vyote nchini vinapata hatia za umiliki ili kupunguza changamoto za uvamizi ambazo zimekuwa zikifanywa na wananchi wanaoishi pembezoni mwa viwanja hivyo.

Aidha Naibu Waziri Kihenzile ameipongeza TAA kwa kuendelea kuhakikisha utoaji wa huduma wa huduma katika viwanja vya ndege nchini unaboreshwa hali inayosababisha ongezeko la abiria, mizigo na mashirika ya ndege yanayotoa huduma katika viwanja nchini.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Songea Kapenjama Ndile ameishukuru Serikali kwa kufanya maboresho katika kiwanja hicho kwani yamechochea kukua kwa uchumi wa mkoa huo sababu kukamilika kwake kumekuwa na ongezeko la usafirishaji wa mizigo hususani ya mboga mboga na matunda yanayozalishwa mkoani hapo.

Naye Meneja wa Kiwanja hicho Mhandisi Danstan Komba amesema kukamilika kwa ujenzi wa Barabara ya kuruka na kutua ndege (Run way), taa za kuongozea ndege, uzio, maegesho ya ndege, barabara ya kiungio (Taxing Way) na kituo cha nishati kumekifanya kiwanja hicho kuongeza wigo wa utoaji wa huduma ikiwemo kutumika kwa saa ishirini na nne (24).

Mhandisi Komba amemuhakikishia Naibu Waziri Kihenzile kuwa TAA itachukua hatua stahiki dhidi ya Mkandarasi huyo ili kuhakikisha mradi wa jengo la abiria unakamilika na kurahisisha utoaji wa huduma za abiria wanaotumia kiwanja hicho.

Katikati ni Naibu Waziri wa Wizara ya Uchukuzi, Mhe. David Kihenzile akimsikiliza Meneja wa Kiwanja cha Ndege cha Songea, Mhandisi Danstan Komba (kushoto), kuhusu maendeleo ya miradi mbalimbali inayotekelezwa katika cha Ndege cha Songea, wakati Naibu Waziri huyo alipokagua Kiwanja cha Ndege 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.