Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Stephen Wasira , ametoa wito mzito kwa wananchi wa Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma kulinda amani ya Taifa, akisisitiza kuwa Watanzania wasikubali kugawanywa kwa misingi ya dini, kabila au itikadi. “Akitokea mtu anayetaka kuvunja amani, tumwambie namba aliyopiga haipatikani,” alisema kwa msisitizo mkubwa.
Wasira mesema Tanzania ina historia ya kipekee barani Afrika kwa kuhimiza mshikamano wa kitaifa, akitaja mafanikio makubwa ya CCM katika kuondoa ubaguzi wa aina yoyote na kuimarisha umoja miongoni mwa Watanzania.
Ameeleza kuwa mshikamano wa kitaifa ni zawadi ya pekee kutoka kwa Mungu ambayo haipaswi kupuuzwa wala kuvurugwa.
Katika mkutano huo, Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Kanali Ahmed Abbas Ahmed, alitumia nafasi hiyo kumshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuimarisha miundombinu muhimu, ikiwemo ujenzi wa barabara na bandari katika Wilaya ya Nyasa.
Alibainisha kuwa mkandarasi wa barabara ya Mbamba Bay – Ndumbi na Litui – Kitai tayari yupo kazini.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Ruvuma, Komred Oddo Mwisho, alieleza kuwa Serikali imetoa Sh bilioni 22 ajili ya ujenzi wa daraja la Mto Mitomoni , litakalounganisha Wilaya ya Nyasa na Songea Vijijini, jambo litakalorahisisha usafiri na kukuza maendeleo ya kiuchumi.
Tayari serikali I melisanifu daraja la mitomoni na Mkandarasi ameshapatikana
Regional Commissioner Office
Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.
Simu: 0252602256
Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174
Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz
Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.