• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

NAMTUMBO yawapiga jeki,wanawake,vijana na wenye ulemavu milioni 172

Imewekwa kuanzia tarehe: June 8th, 2021

Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo Mkoani  Ruvuma  kwa kipindi cha miaka sita 2015/2016  hadi  2020/2021 imekopesha  vikundi 229 wenye  wanachama  zaidi ya 800 jumla ya shilingi  milioni 172,500,000.

Afisa  maendeleo ya jamii wa Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo bwana  Peres  Kamugisha aliyasema hayo kwenye semina elekezi  ya ujasilimali na maendeleo ya biashara  kwa vikundi vilivyopatiwa mkopo katika halmashauri hiyo.

Bwana Kamugisha alisema  halmashauri imelazimika kutoa semina elekezi  kwa vikundi vilivyopatiwa mkopo ili kuwa na uelewa  kuhusu namna  ya kufanya  shughuli za  ujasiliamali na kuwa na maendeleo  ya kweli katika biashara zao  na waweze kulipa mikopo  wanayopewa kadiri ya sheria ya mikopo  za mwaka 2021.

Alisema  zipo changamoto kubwa ya  baadhi ya vikundi  kutokuwa na uaminifu  na kupelekea  kutorejesha mikopo kwa wakati  licha ya kuwapatia semina elekeza ya ujasiliamali pamoja na namna  ya kuendesha biashara  zao mara kwa mara.

Mkuu wa wilaya ya Namtumbo Sophia Mfaume Kizigo alialikwa katika semina hiyo na kuwataka wanufaika ya mikopo ya vikundi vya wanawake,vijana na watu wenye ulemavu kuzitumia fedha hizo  katika malengo yaliyokusudiwa .

Kizigo alidai wapo wanaopata mkopo na hawataki kurudisha hali inayokwamisha vikundi vingine vyenye uhitaji wa kupata mikopo hiyo kukosa kupatiwa mikopo kutokana na baadhi ya vikundi kutokuwa waaminifu wa kurudisha mikopo.

Wapo  walemavu wanaowezeshwa kupata mikopo ili wajiinue kimapato lakini wapo wengine wanatumia kigezo hicho cha ulemavu kama kinga ya kutorudisha  mikopo na wanaposhindwa kurudisha mikopo wanajizuia kupata mkopo tena .

Aliwataka  walemavu  kutojiona kuwa wao ni tofauti na makundi mengine bali kuwa wao ni sawa na makundi mengine na wanatakiwa kupata mikopo na kuirudisha ili waendelee kuaminiwa na serikali na  kukopeshwa mara kwa mara.

Asha  kamtende ni mnufaika wa mkopo kutoka katika kikundi cha wajasiliamali nguvu moja pamoja na kuishukuru serikali kuwajali wajasiliamali wadogo kwa kuwapatia mikopo alisema  kikundi chao kimewezeshwa kupata 1,500,000 na wataitumia fedha hiyo kwa malengo yaliyokusudiwa na kasha kurudisha mkopo huo kwa wakati  ili serikali iwaamini na kisha kuendelea kukopeshwa mara kwa mara.

Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo  kwa mwaka fedha  2020/2021 hadi mei  halmashauri imetoa kiasi cha shilingi   80,000,000 kupitia mapato yake  ya ndani kwa vikundi 25 vya wanawake ,vijana na watu wenye ulemavu  vyenye jumla  ya wanachama 60 ambapo kwa miaka sita jumla ya shilingi milioni 172,500,000 zimekopeshwa kwa vikundi vya vijana 94, vyenye wanachama310 vimepatiwa mkopo wa shilingi 168,800,000,vikundi vya watu wenye ulemavu vikundi 26 vyenye wanachama zaidi ya 70 jumla ya shilingi 47,000,000  zilikopeshwa  na saccos ya vijana moja jumla ya shilingi 5,350,000.

Imetolewa na Afisa Habari wilaya ya Namtumbo

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.