• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

NAUYE afurahishwa na kasi ya zoezi la Anwani za Makazi na Postikodi Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: April 13th, 2022

Waziri wa Habari Mawasiliano na Teknolojia   Nape Nauye ameupongeza Mkoa wa Ruvuma kwa kasi ya zoezi la uandikishwaji wa anwani za makazi na Postikodi linaloendelea kitaifa.

Akizungumza mara baada ya kusomewa taarifa ya Mkoa na Mtehama wa Mkoa huo Yahya Madenge katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa  amesema iko katika asilimia 97.

Nauye amefanya ziara Mkoani humo ya siku moja  na kujionea utekelezwaji wa kasi na kueleza umuhimu wa anwani za makazi kuwa zoezi hilo  litaleta manufaa katika Taifa kwa kuitambulisha Ramani ya Tanzania Kimataifa.

 “Serikali imeona umuhimu wa kufanya zoezi hilo  kwaajili ya kuitangaza inchi ya Tanzania pamoja na  kurahisisha mawasiliano kwa mataifa mbali mbali”.

Hata hivyo Nauye  ametoa wito kwa uongozi wa Mkoa na wananchi kuwa zoezi hilo litumike kuifadhi historia ya Mkoa huo na Taifa kwa ujumla ikiwemo vizazi vijavyo ziweze kujua historia  kupitia majina ya mitaa na Barabara.

Mkuu Mkoa  wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge amesema namna Mkoa wa Ruvuma unavyotekeleza zoezi la anwani za makazi na kufikia asilimia 97 na kushika nafasi ya 10 Kitaifa.

Ibuge amesema katika kuendesha zoezi hilo la anuani za Makazi Katika Halmashauri linatarajia kuisha April 15 na kuwasilisha taarifa kwenyekanzidata na kuweka vibao pamoja na namba kwenye makazi  na Kitaifa April 30.

Ibuge amewapongeza wananchi wa Mkoa huo kwa namna ambavyo wameona ushirikiano kwa kupendekeza majina ya Mitaa yakiwemo ya Viongozi na kujitoa kugharamia pale panapohitaji gharama na kuongeza nguvu kwa kuhakikisha zoezi linakwenda vizuri.

Hizi nguzo tunazoziweka ni zoezi litakalokuwa endelevu, ndugu wananchi wa Mkoa wa Ruvuma zikalindwe tutoke kwenye ujima na ushamba wa nguzo kwa “sababu ni chuma na kuona  chuma chakavu hiyo nayo ni  kipimo kingine ambacho tutakuwa tumejishusha” 

Imeandaliwa na Aneth Ndonde pamoja  Jackson Mbano

Kutoka Kitengo Cha Habari na Mawasiliano Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma

April 13,2022. 

 

 

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru wamulika maendeleo Nyasa

    May 12, 2025
  • MWENGE wa Uhuru 2025 waikubali miradi yote Mbinga

    May 12, 2025
  • WANANCHI walivyojitokeza kuupokea mwenge wa Uhuru katika kijiji cha Maguu Mbinga

    May 11, 2025
  • MAHABA ya wananchi wa Mbuji wilayani Mbinga kwa Mwenge wa Uhuru 2025

    May 11, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.