• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

NMB yatoa madawati 150 ya milioni 16 Songea

Imewekwa kuanzia tarehe: June 5th, 2025


Benki ya NMB imetoa madawati 150 yenye thamani ya shilingi milioni 16.5 kwa shule  tatu za msingi katika Halmashauri ya Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma.

Shule ambazo zimepatiwa madawati hayo ni Shule ya Msingi Matimira, Magagura na Magima, ambapo kila shule imepata madawati 50 yenye thamani ya shilingi milioni 5,500,000.

Katibu Tawala wa Wilaya ya Songea, Mtela Mwampamba, akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Songea Mhe. Kapenjama Ndile wakati wa makabidhiano ya madawati hayo yaliyofanyika katika shule ya msingi Matimira, ameishukuru benki ya NMB kwa kutumia kiasi kikubwa cha fedha kwa ajili ya kupunguza kero ya upungufu wa madawati kwa wanafunzi wanaosoma katika shule hizo.

Naye Kaimu Meneja wa NMB Kanda ya Kusini, Roman Degeleki, amesema benki ya NMB ni wadau wa elimu wanaotambua  juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia za kusimamia upatikanaji wa huduma bora za Elimu hivyo  wana wajibu wa kuunga mkono juhudi za Serikali ili kuboresha sekta hiyo.

Ameeleza kuwa changamoto za sekta ya Elimu kwa benki ya NMB ni jambo la kipaumbele, na walipopata maombi ya kuchangia maendeleo ya elimu katika shule hiyo walifarijika kwa kuwa sekta ya Elimu ndio chachu ya maendeleo katika jamii.

Ameongeza kuwa benki ya NMB imekuwa mstari wa mbele kuchangia huduma za kijamii kwa lengo la kurejesha sehemu ya faida kwa jamii akibainisha kwa zaidi ya miaka nane mfululizo wamekuwa wakitenga asilimia 1 ya faida kama sehemu ya uwajibikaji kwa jamii inayowazunguka.

Akisoma taarifa ya shule ya msingi Matimira, Mwalimu Renista Vungu, amesema shule hiyo ilikuwa ikikabiliwa na changamoto ya uhaba wa madawati, kutokana na ongezeko kubwa la wanafunzi, ambao kwa sasa wapo 810.  

Kwa mujibu wa Mwalimu Vungu, shule hiyo ilikuwa na mahitaji ya madawati 256, huku yaliyokuwepo yakiwa 190 pekee, hivyo kulikuwa na upungufu wa madawati 66, ambapo kupitia ufadhili wa benki ya NMB, shule imepokea madawati 50, hatua ambayo itapunguza kwa kiasi kikubwa changamoto hiyo.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Mhe. Menans Komba, amewataka walimu wa shule hizo kusimamia ipasavyo matumizi ya madawati ili yaweze kudumu kwa muda mrefu akiwasihi wanafunzi kuyalinda na kuepuka kuyaathiri kwa namna yoyote, kwani yamepatikana kwa lengo la kuwasaidia katika safari yao ya elimu.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • NMB yatoa madawati 150 ya milioni 16 Songea

    June 05, 2025
  • UCHANGIAJI damu wazidi kuimarika Ruvuma

    June 04, 2025
  • TRILIONI 1.18 za Rais Samia zavunja ukame wa maendeleo Ruvuma,ndani ya miaka minne Ruvuma yachanua

    June 04, 2025
  • RAS RUVUMA alivyowaongoza wananchi kuchangia damu

    June 04, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.