• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

REDIO Hekima Mbinga yazinduliwa Rasmi na Kiongozi wa Mbio za Mwenge Lt Mwambashi

Imewekwa kuanzia tarehe: September 4th, 2021

MRADI wa Kiwanda cha vijana Chipukizi umezinduliwa  pamoja na Mradi wa Redio Hekima FM 102.7 na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Lt.Josephine Mwambashi.

Akitoa Taarifa ya kikundi cha Vijana Mwenyekiti wa Kikundi cha Chipukizi Keneth Mbena amesema kikundi cha vijana Kata ya Kigonsera kilisajiliwa mwaka 2019 kikiwa na idadi ya wanachama 6 wenye umri kuanzia miaka 18 hadi 35.

Akielezea lengo la kuanzisha mradi huo ni kuongeza wigo wa ajira ambapo jumla ya wanufaika 15 wamejipatia ajira na kujiongezea kipato kupitia asilimia 10 ya mapato ya ndani.

Hata hivyo Mbena amesema kikundi hicho cha vijana chipukizi kimefanikiwa kupata mkopo kutoka mfuko wa marejesho  wenye zaidi ya shilingi milioni 22 na kununua mashine  ya kuchanganya Saruji.

“Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru hadi kufikia Agosti 5,2021 wanakikindi tumefanikiwa kufyatua tofali 30,000 kwaajili ya ujenzi wa Jengo la ofisi ya  Halmashauri na kupatiwa malipo ya shilingi milioni 9”.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa amekipongeza kwa kuamua kuunda kikundi na kufanya ujasiliamali na kuepuka kujiunga na  makundi ya mtaani na kujiingiza katika madawa ya kulevya,na kuwapatia vijana wengine ajira.

 Mwambashi ametoa rai kwa vijana kuendelea kuchangamkia fursa na kuacha kuwa tegemezi zaidi wawe wabunifu ili kuweza kujikwamua kiuchumi katika familia na kurejesha mkopo kwa wakati ili wengine nao wapate kupata mkopo huo.

Kwa upande wake  Askofu Mkuu wa Jimbo la Mbinga  John Ndimbo amesema mradi huo umejengwa kwa  kushirikiana na waumini  wa Jimbo la Mbinga  na ufadhili toka Jimbo ndugu(Wiirzburg) na kugharimu zaidi ya milioni 160.

Ndimbo amesema mradi huo ulianza kujengwa mwaka 2018 na kukamilika mwaka 2019 na kuanza kufanya kazi Oktoba  4,2019,na inasikika katika maeneo ya Wilaya ya Mbinga,Nyasa pamoja na maeneo ya Wilaya ya Songea.

Askofu Mkuu ameelezea Malengo ya kuanzishwa kwa redio hii ni pamoja na kutengeneza jamii yenye hofu ya Mungu ili iwezekuishi kwa amani na mshikamano,kukuza maadili katika makundi mbalimbali pamoja na kuhamasisha jamii kujikwamua kiuchumi.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka Ofisi ya Habari Mkoa wa Ruvuma

Septemba 4,2021.

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.